Rais Samia aongoza harambee uchangiaji ujenzi kituo cha watoto, achangia milioni 150

Na Mwandishi Wetu

Rais  Samia Suluhu Hassan ameongoza Harambee ya kuchangia ujenzi wa Kituo cha Watoto wenye mahitaji Maalum cha Bagamoyo Diaconic Lutheran Centre ambapo amechangia  Sh 150 milioni, kwa ajili ya ujenzi wa  kituo hicho  cha Watoto wenye mahitaji maalumu kinachotarajiwa kujengwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani mkoani Pwani.

Pia washauri wa Rais wamechangia Sh 100  milioni, hivyo kufanya ofisi ya Rais kuchangia  Sh 250 kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho.

Akizungumza katika Harambee hiyo Rais Samia amemhakikishia Mkuu wa Kanisa hilo, Askofu Dk Alex  Malasusa  kuwa serikali itaendelea kushirikiana bega kwa bega katika hatua zote za ujenzi pamoja na uendeshaji wa kituo hicho.

“Kiwango nilichojiwekea kuchangia katika shughuli za kanisa ni Sh  milioni 100, lakini nikivaa kofia ya bibi nitachangia  Sh milioni 50, na wasaidizi wangu wamejichanga na kuchangia Sh milioni 250, hivyo kama ofisi yangu tunachangia Sh milioni 250,”

Aidha Rais Samia amesisitiza kuwa matendo chanya yanayofanywa na baadhi ya watumishi wa dini yanaonyesha mfano bora kwa wengine wanaojiita watumishi wa dini, lakini hawaleti manufaa kwa jamii.

Pia amehimiza ushirikiano wa wazazi wote wawili katika malezi ya watoto wenye changamoto, akisema ni jukumu la familia nzima.

“Nasimama mbele yenu kama mama ambaye nabeba dhamana ya malezi kama mama, si tu wa mahaitaji maalumu bali wote, ninasimama nikiwa naelewa fika jukumu kubwa wanalolibeba akina mama wanapokuwa na watoto wenye uhitaji maalumu,” amesema Rais Samia.

Ameeleza dhamira ya Serial kuendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo wakiwamo viongozi wa  dini na mashirika yasiyo ya kiserikali, kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora kwa watoto  wenye mahitaji.

Kwa upande wake Mkuu wa KKKT, Askofu Dk Alex Gehaz Malasusa amemshukuru Rais Samia kwa mchango wake na uwepo wake katika harambee hiyo akisema unaleta ujumbe kwamba walemavu ni sehemu ya taifa na wanahaki ya elimu na kujifunza.

Amesema tayari kanisa hilo limeanza michoro ya usanifu wa majengo na imekamilika, huku ikikusanya Sh 2.7 bilioni kupitia harambee ya ndani iliyojumuisha sharika na mitaa mbalimbali.

spot_img

Latest articles

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

More like this

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...