Yanga haina imani na TFF, Bodi ya Ligi, yasisitiza haichezi Dabi

Na Mwandishi Wetu

Uongozi wa Klabu ya Yanga umesema hauko yatari kupeleka shauri kwenye Kamati za Mamlaka za soka  ndani  kama iliyoelekezwa na Mahakama ya  Kimataifa ua Usuluhisi wa Michezo (CAS), ikihofia dhuluma, huku ikisisitiza kutocheza mechi ya’derby’.

CAS ilielekeza Yanga  kurudi kwenye Kamati za ndani kabla ya kurudi katika mahakama hiyo kwa ajili ya rufani.

Katika taarifa ambayo klabu hiyo imeitoa leo   Mei 5, 2025imesema  msimamo wao juu ya mchezo namba 184 wa Ligi Kuu Bara uko pale pale wa kutoshiriki mechi hiyo kwa namna yoyote.

“Kutokana na uonevu na uvunjwaji mkubwa wa kanuni na upendeleo wa dhahiri kwa baadhi ya  timu unaondelea kufanywa na Mamlaka za soka  Tanzania, Uongozi wa Yanga hauna imani na hauko tayari kupeleka shauri hilo kwenye Mamlaka ambao zinatenda dhulma,” imesema.

Kupitia Taarifa hiyo,uongozi wa Wanajangwani hao,umewataka Wanayanga kuwa tayari kuipambania haki yao kivyovyote vile ili kukomesha dhuluma na uvunjwaji wa kanuni unaondelea  kwa maslahi mapanda ya soka nchini.

Ikumbukwe kuwa Yanga ilifungua shauri la madai CAS  kwa kutoridhishwa na kitendo cha kuahirishwa kwa mchezo wake dhidi ya Simba uliokuwa uchezwe Machi 8, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Yanga iliwasilisha shauri la kuomba mechi hiyo isipangiwe tarehe nyingine hadi uamuzi utakapotolewa na Makahama hiyo. Kesi hiyo imefunguliwa dhidi ya  Shirikisho la Soka Tanzania(TFF), Bodi ya Ligi Kuu Tanzania na Klabu ya Simba.

Hata hivyo CAS iliijibu Yanga kwa kuitaka kurudi katika Kamati za Mamlaka za soka ambapo muda mfupi baadaye Bodi ya Ligi ilitangaza kutoa ratiba mpya ya  Ligi Kuu ikiwamo mchezo huo uliahirishwa wa Yanga na Simba.

spot_img

Latest articles

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

More like this

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...