Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco afariki dunia kwa ajali

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Usambazaji Umeme Tanzania (TANESCO) Gissima Nyamo-Hanga amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo Aprili 13, 2025 kwa ajali iliyotokea Wilayani Bunda mkoani Mara.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Evansi Mtambi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo amefafanua kuwa tukio limetokea kati ya saa 6 hadi 7 usiku wa kuamkia leo.

“Ni kweli tukio lipo na Gissima amefariki Dunia na RPC atakuwa na taarifa kwa kina,” amesema Mtambi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Pius Lutumo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akiahidia kutoa taarifa kwa kina badae kidogo.

Naye Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mara Nicksoni Babu amebainisha kuwa Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali Teule Wilaya ya Bunda huku wakisubiria taarifa zaidi na taratibu nyingine.

Media Brains inatoa pole kwa Menejimeti ya Tanesco ndugu, jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha kumpoteza mpendwa wao.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...