Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco afariki dunia kwa ajali

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Usambazaji Umeme Tanzania (TANESCO) Gissima Nyamo-Hanga amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo Aprili 13, 2025 kwa ajali iliyotokea Wilayani Bunda mkoani Mara.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Evansi Mtambi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo amefafanua kuwa tukio limetokea kati ya saa 6 hadi 7 usiku wa kuamkia leo.

“Ni kweli tukio lipo na Gissima amefariki Dunia na RPC atakuwa na taarifa kwa kina,” amesema Mtambi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Pius Lutumo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akiahidia kutoa taarifa kwa kina badae kidogo.

Naye Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mara Nicksoni Babu amebainisha kuwa Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali Teule Wilaya ya Bunda huku wakisubiria taarifa zaidi na taratibu nyingine.

Media Brains inatoa pole kwa Menejimeti ya Tanesco ndugu, jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha kumpoteza mpendwa wao.

spot_img

Latest articles

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi Timu ya Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa...

‎Msigwa: Bwawa la Kidunda ni mradi wa kimkakati kwa Maji, Kilimo na Nishati

Na Mwandishi Wetu Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ameipongeza Wizara ya Maji kwa...

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

More like this

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi Timu ya Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa...

‎Msigwa: Bwawa la Kidunda ni mradi wa kimkakati kwa Maji, Kilimo na Nishati

Na Mwandishi Wetu Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ameipongeza Wizara ya Maji kwa...