YANGA YAIBAMIZA AZAM, TABORA HALI TETE, COASTAL YAZINDUKIA MKWAKWANI

Na Mwandishi Wetu

Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC katika mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo mabao ya Yanga yalifungwa na Pacome Zouzoua dk 11, Prince Dube dk 34 wakati la Azam likifungwa na Lusajo Mwaikenda dk 81.

Wakati huo huo timu ya Tabora United imepoteza mchezo wa nne mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya leo Aprili 10, 2025 kufungwa mabao 3-0 na Mashujaa FC katika kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.

Kabla ya mchezo wa leo ilitoka kufungwa na Pamba 1-0, CCM Kirumba, Mwanza, imepoteza nyumbani dhidi ya Yanga 3-0, na JKT Tanzania iliifunga 2-1.

Nayo Coastal Union baada ya kukosa ushindi katika michezo nane mfululizo leo imezinduka kwa kuifunga Singida BS mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga.

spot_img

Latest articles

“MADEREVA TANESCO KUWENI CHACHU UTOAJI HUDUMA BORA”

📌Watakiwa kutunza vyombo vya usafiri ili kuongeza ufanisi wa huduma 📌TANESCO yanunua vyombo vya usafiri...

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

More like this

“MADEREVA TANESCO KUWENI CHACHU UTOAJI HUDUMA BORA”

📌Watakiwa kutunza vyombo vya usafiri ili kuongeza ufanisi wa huduma 📌TANESCO yanunua vyombo vya usafiri...

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...