YANGA YAIBAMIZA AZAM, TABORA HALI TETE, COASTAL YAZINDUKIA MKWAKWANI

Na Mwandishi Wetu

Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC katika mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo mabao ya Yanga yalifungwa na Pacome Zouzoua dk 11, Prince Dube dk 34 wakati la Azam likifungwa na Lusajo Mwaikenda dk 81.

Wakati huo huo timu ya Tabora United imepoteza mchezo wa nne mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya leo Aprili 10, 2025 kufungwa mabao 3-0 na Mashujaa FC katika kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.

Kabla ya mchezo wa leo ilitoka kufungwa na Pamba 1-0, CCM Kirumba, Mwanza, imepoteza nyumbani dhidi ya Yanga 3-0, na JKT Tanzania iliifunga 2-1.

Nayo Coastal Union baada ya kukosa ushindi katika michezo nane mfululizo leo imezinduka kwa kuifunga Singida BS mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga.

spot_img

Latest articles

Natoa nishani ya uthubutu kwa Kanisa Katoliki 2025

Siyo hulka yangu kujadili masuala ya dini katika chambuzi ninazofanya. Wala, sikusudii kujikita kuibua...

Benki ya CRDB yafunga mwaka kwa kukabidhi zawadi ya magari kwa washindi wa Simbanking

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB, imemkabidhi Deo Ferdinand Mlawa na wenzake watano zawadi...

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

More like this

Natoa nishani ya uthubutu kwa Kanisa Katoliki 2025

Siyo hulka yangu kujadili masuala ya dini katika chambuzi ninazofanya. Wala, sikusudii kujikita kuibua...

Benki ya CRDB yafunga mwaka kwa kukabidhi zawadi ya magari kwa washindi wa Simbanking

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB, imemkabidhi Deo Ferdinand Mlawa na wenzake watano zawadi...

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...