SIMBA YAIFUATA AL MASRY NA HESABU KALI

Na Winfrida Mtoi

Kikosi cha Simba kinatarajia kuondoka Machi 28,2025 kuifuata timu ya Al Masry nchini Misri kwa mchezo wao wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika huku uongozi wa klabu hiyo ukiwa na hesabu za kutinga nusu fainali.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Habari na Mawasiliano wa hiyo, Ahmed Ally amesema malengo yao msimu huu ni kuhakikisha wanavuka hatua ya robo fainali na kutinga nusu fainali.

Ahmed amesema licha ya kukutana na mpinzani mgumu hatua ya robo fainali lakini wamejipanga kuhakikisha wanavuka na ndiyo sababu ya kuja na kauli mbiu ya ‘Hii tunavuka’.

“Kwa miaka mitano mfululizo tumekuwa tukiishia robo fainali kwenye michuano ya Afrika lakini safari hii tumedhamiria kuhakikisha tunavuka,”amesema Ahmed.

Aidha amesema wachezaji waliokuwa sehemu ya timu ya taifa, Taifa Stars, wataungana na wenzao nchini Misri ili kukamilisha maandalizi ya mchezo huo wakati Camara na Mukwala, tayari wamewasili na kuungana na wenzao kwa maandalizi zaidi kabla ya safari.

spot_img

Latest articles

Rostam Azizi aeleza jinsi alivyoshirikisha wadau kuunda mfumo imara wa vyombo binafsi vya habari

Na Mwandishi Wetu Mfanyabiasha   Rostam Azizi ameeleza  mbinu waliyotumia kuhakikisha tasnia ya habari inaimarika nchini...

Wachezaji wawili Yanga wageukia masumbwi, kuzichapa Julai 26 Dar

Na Winfrida Mtoi Wachezaji wa Yanga, Kibwana Shomari na Denis Nkane wamajitosa kwenye mchezo wa...

Watendaji Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 wafundwa

Na Mwandishi wetu TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imewaasa watendaji wa uchaguzi...

Prof. Kabudi: Anayefanya kazi bila ‘Press Card’ anavunja Sheria

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi amesema...

More like this

Rostam Azizi aeleza jinsi alivyoshirikisha wadau kuunda mfumo imara wa vyombo binafsi vya habari

Na Mwandishi Wetu Mfanyabiasha   Rostam Azizi ameeleza  mbinu waliyotumia kuhakikisha tasnia ya habari inaimarika nchini...

Wachezaji wawili Yanga wageukia masumbwi, kuzichapa Julai 26 Dar

Na Winfrida Mtoi Wachezaji wa Yanga, Kibwana Shomari na Denis Nkane wamajitosa kwenye mchezo wa...

Watendaji Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 wafundwa

Na Mwandishi wetu TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imewaasa watendaji wa uchaguzi...