Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed

GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali ya uchumi wa Tanzania imeendelea kuimarika na kuwa himilivu.

Gavana Tutuba ameyasema hayo Machi, 20 2025 jijini Dar es Salaam katika hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa wananchi na wadau mbalimbali.

Imefanyika makao makuu ya BoT jijini Dodoma, makao makuu ndogo Zanzibar, matawi ya Mtwara, Mwanza, Arusha na Mbeya.

“Mpaka sasa, Tanzania imeendelea kung’ara katika medali za kiuchumi kidunia. Hali yetu ya uchumi, imeendelea kuwa nzuri katika sekta mbalimbali ikiwemo Sekta ya Fedha ambayo imeendelea kuimarika, imeendelea kuwa na utulivu, imeendelea kuwa thabiti.

“Imeendelea kuwa na mtaji mkubwa na ukwasi wa kutosha na pia ina ufanisi mzuri wa viwango vya kimataifa na inajiendesha kwa faida,” amesema Gavana Tutuba.

Amesema, kwa kipindi cha miaka mitatu Sekta ya Uchumi na Fedha nchini imeendelea kufanya vizuri.

“Na kwa takwimu tunafahamu kwamba, kwa mwaka 2024 uchumi wa nchi yetu ulikuwa kwa takribani asilimia 5.4 ikilinganishwa na ukuwaji wa uchumi wa kidunia ambao ulikuwa asilimia 3.2.Kwa hiyo tumefanya vizuri,” amesema.

Aidha, kwa upande wa mfumuko wa bei, Gavana Tutuba amesema ulikuwa asilimia 3.1 ukilinganishwa na mfumuko wa bei wa kidunia wa asilimia 4.7.

Kwa upande wa ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi, Gavana Tutuba amesema, mambo yalikuwa mazuri, kwani likuwa kwa asilimia 16.8 ikilinganishwa na lengo la asilimia 15.

Kutokana na changamoto hiyo, Gavana Tutuba ametoa wito kwa wananchi wote kujiepusha na shughuli za upatu.

Pia, amewataka wananchi kuhakikisha wanapata huduma za mikopo kwa watoa huduma wenye leseni halali kutoka Benki Kuu au kupitia taasisi zilizokasimishwa mamlaka.

“Kwenye halmashauri kwa leseni za VICOBA na kwenye Tume ya Maendeleo ya Ushirika kwa leseni za SACCOS,” amesema.

Pia, amewataka watoa huduma za mikopo wenye leseni kuhakikisha wanatoa huduma sahihi na ambazo haziwaumizi wananchi.

Amesema, kwa yule ambaye atakwenda kinyume na leseni yake, Benki Kuu itachukua hatua ikiwemo kumfutia leseni husika.

Kuhusu mfungo, Gavana Tutuba amesema, kwa upande wa kiroho, viongozi wengi wa kidini zote za Kiislamu na Kikristo wameendelea kufundisha hiki ni kipindi muhimu ambacho mwanadamu anapaswa kumrejea Mungu wake.

“Kipindi hiki cha mfungo ninafahamu ni kipindi muhimu sana katika maisha ya mwanadamu na kipindi ambacho kina faida nyingi za kiroho na kimwili. Ni kipindi ambacho kinatupatia fursa na Mwenyezi Mungu kwa sala, maombi na hata kutafakari ukuu wa Mwenyezi Mungu,” amesema.

Naye Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania, Dkt. Abubakar Zuber, ameitaka Benki Kuu kuendelea kutoa elimu ya fedha kwa wananchi ili kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi katika matumizi ya huduma za fedha.

Amesema, kupitia elimu ya fedha kwa wananchi itawapa uwanda mpana wa kuweza kutambua sehemu sahihi za kupata mikopo.

Pia, amesema elimu hiyo itasaidia wananchi kuendesha biashara zao kwa faida.

“Kwa hiyo msiache kutoa elimu hii, ili iweze kufikia mahali ambapo mwananchi anaweza kufanya shughuli zake kwa utulivu,” amesema.

Amewahimiza wananchi kuendelea kudumisha amani nchini hasa kipindi hiki Taifa linaelekea katika Uchaguzi Mkuu.

spot_img

Latest articles

DAWASA KUFANYA MATENGENEZO KINGA, MAJI KUKATIKA KWA SAA 12

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

OTR kuongeza kasi ya mageuzi ili kukuza tija ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejizatiti kuongeza kasi ya mageuzi ya...

Mikono ya Kitanzania, Gesi ya Tanzania: Bomba la Gesi kutoka Kisemvule–Mbagala Linaenda Kasi

Kampuni ya Rashal Energies Limited, chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Farhiya Warsame, yajenga bomba...

SAPP kufungua Fursa kwa Tanzania Kuwa Kitovu cha Biashara ya Umeme Kusini mwa Afrika

📌Nchi 18 Zakutana Zanzibar kujadili usalama wa nishati ya umeme kusini mwa Afrika 📌Kuuza au...

More like this

DAWASA KUFANYA MATENGENEZO KINGA, MAJI KUKATIKA KWA SAA 12

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

OTR kuongeza kasi ya mageuzi ili kukuza tija ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejizatiti kuongeza kasi ya mageuzi ya...

Mikono ya Kitanzania, Gesi ya Tanzania: Bomba la Gesi kutoka Kisemvule–Mbagala Linaenda Kasi

Kampuni ya Rashal Energies Limited, chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Farhiya Warsame, yajenga bomba...