Derby ya wanawake kesho, ubabe ubabe

Na Winfrida Mtoi

Simba Queens na Yanga Princess kesho Machi 18,2025 zinashuka dimbani katika mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara, kwenye Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Kila mmoja akionekana kuwa na hamu ya  kuondoka na alama zote tatu ambapo Yanga Princess inahitaji kulipa kisasi ya kipigo cha bao 1-0 ilichopokea katika mechi ya mzunguko wa kwanza, huku Simba Queens ikitaka kuendeleza ubabe mbele ya wadada hao wa Jangwani.

Simba Queens ambayo ni mwenyeji wa mchezo huo, inaongoza katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 34 wakati Yanga ikiwa nafasi ya tatu na alama 24 zote zikicheza mechi 12.

Akizungumzia mchezo huo kocha mkuu wa Simba Queens, Yussif Basigi amesema ni mechi muhimu kwao kutokana na kila mmoja kuitolea macho, huku akihitaji ushindi ili kuendelea kukaa kileleni kwa sababu wamepishana alama mbili na JKT Queens iliyopo nafasi ya pili.

Kwa upande wake kocha mkuu wa Yanga Princess, Edna Lema, ametamba kuwa licha ya wapinzani wao kuwa kwenye ubora na kuongoza ligi lakini  wamejiandaa vizuri na hawana presha.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...