RAIS MWINYI:TUSIPANDISHE BEI ZA BIDHAA ZA VYAKULA WAKATI WA RAMADHANI

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi ameeleza kuridhishwa na upatikanaji wa bidhaa za vyakula na kuwataka wafanyabiashara kutopandisha bei wakati Ramadhani itakapoanza.

Rais Dk.Mwinyi amesema hayo alipotembelea Masoko ya Jumbi, Mwanakwerekwe na Darajani kuangalia mwenendo wa biashara na upatikanaji wa bidhaa za vyakula kuelekea mwezi wa Ramadhani.

Ameeleza kuwa Serikali inajipanga kwa ajili ya Ujenzi wa Masoko mengine maeneo mbalimbali ili kila mfanyabiashara afanye biashara kwenye mazingira rasmi .

Kuhusu usafi wa masoko ameuagiza uongozi wa masoko hayo kutafuta njia bora zaidi ya uhifadhi wa bidhaa za wafanyabiashara ili masoko kuwa safi wakati wote.

Amezielekeza taasisi zinazosimamia masoko hayo kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya maji na vipooza hewa katika masoko yote pamoja na kuimarisha usafi.

Ziara hiyo ya Rais Mwinyi ni ya kwanza tangu kufunguliwa kwa masoko mapya ya Jumbi , Mwanakwerekwe na ukarabati mkubwa wa Soko la Darajani.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

More like this

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...