RAIS MWINYI:TUSIPANDISHE BEI ZA BIDHAA ZA VYAKULA WAKATI WA RAMADHANI

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi ameeleza kuridhishwa na upatikanaji wa bidhaa za vyakula na kuwataka wafanyabiashara kutopandisha bei wakati Ramadhani itakapoanza.

Rais Dk.Mwinyi amesema hayo alipotembelea Masoko ya Jumbi, Mwanakwerekwe na Darajani kuangalia mwenendo wa biashara na upatikanaji wa bidhaa za vyakula kuelekea mwezi wa Ramadhani.

Ameeleza kuwa Serikali inajipanga kwa ajili ya Ujenzi wa Masoko mengine maeneo mbalimbali ili kila mfanyabiashara afanye biashara kwenye mazingira rasmi .

Kuhusu usafi wa masoko ameuagiza uongozi wa masoko hayo kutafuta njia bora zaidi ya uhifadhi wa bidhaa za wafanyabiashara ili masoko kuwa safi wakati wote.

Amezielekeza taasisi zinazosimamia masoko hayo kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya maji na vipooza hewa katika masoko yote pamoja na kuimarisha usafi.

Ziara hiyo ya Rais Mwinyi ni ya kwanza tangu kufunguliwa kwa masoko mapya ya Jumbi , Mwanakwerekwe na ukarabati mkubwa wa Soko la Darajani.

spot_img

Latest articles

🔴🔴Wizara ya Maliasili yaendelea kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Taasisi zake kwa Kamati za Bunge

📍 Kamati yaipongeza TAWA kwa ubunifu uliopelekea ongezeko la watalii, mapato Na Mwandishi Wetu, Dodoma KAMATI...

JAB yaonya waajiri katika vyombo vya habari kuzingatia Sheria kuepuka migogoro ya kisheria

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewasisitiza waajiri kwenye vyombo...

Kata za Mzinga, Malangali kupiga kura kuchagua madiwani kesho

Na Mwandishi wetu, Dodoma JUMLA ya Wapiga Kura 38,151 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la...

TCAA yapokea ugeni kutoka Wizara Ujenzi na Uchukuzi Zanzibar

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) ikiongozwa na Kaimu Mkurugenzi...

More like this

🔴🔴Wizara ya Maliasili yaendelea kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Taasisi zake kwa Kamati za Bunge

📍 Kamati yaipongeza TAWA kwa ubunifu uliopelekea ongezeko la watalii, mapato Na Mwandishi Wetu, Dodoma KAMATI...

JAB yaonya waajiri katika vyombo vya habari kuzingatia Sheria kuepuka migogoro ya kisheria

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewasisitiza waajiri kwenye vyombo...

Kata za Mzinga, Malangali kupiga kura kuchagua madiwani kesho

Na Mwandishi wetu, Dodoma JUMLA ya Wapiga Kura 38,151 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la...