MAAFISA 26 WA LBL WAKAMATWA DAR

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema kuanzia Februari 18 hadi 22,2025 limewakamata watuhumiwa 26 kwa tuhuma za kujihusisha na biashara haramu ya upatu mtandaoni bila kuwa na kibali kutoka Benki Kuu Tanzania.

Taarifa iliyotolewa na Polisi leo Februari 24,2025, imewataja baadhi ya watuhumiwa hao kuwa ni Najim Issa Houmud Mkurugenzi (34) mkazi wa Kigamboni, Hatibu Kudura (25) mkazi wa Kinondoni, Fatum Hamisi (26) mkazi wa Kigamboni na Athumani Sadik (29) mkazi wa Mabibo.

Taarifa hiyo imesema watuhumiwa hao walikamatwa katika maeneo ya Mbagala, Gongolamboto, Tabata, Mbezi Magufuli, Ubungo Riverside na Mabibo ambapo Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania lilifanya uchunguzi wa kampuni ya LEO BURNETT LONDON (LBL) inayo jihusisha na biashara ya upatu mtandaoni na kubaini kuwa kampuni hiyo haina uongozi maalum.

Vilevile limebaini ufanyaji kazi wake ili uweze kujiunga ni lazima utoe kiasi cha pesa kuanzia sh 50,000 na kuendelea ili uwe mwanachama, pia huchangisha pesa kwa kuwadanganya wananchi kuwa watapata faida kubwa kwa muda mfupi bila ya wanachama kuhusishwa kwa namna yoyote katika shughuli za uendeshaji wa kampuni hiyo.

“Mara upelelezi utakapokamilika watuhumiwa wote watafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma
zinazowakabili, Jeshi la Polisi linatoa wito kwa Wananchi wote kuacha kujihusisha na biashara za upatu mitandaoni bila kujiridhisha kwanza kwa kuwa baadhi ya biashara hizo hazina leseni wala vibali kutoka Mamlaka za kisheria zinazohusika hivyo kuhatarisha usalama pesa zao,” imesema taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Bado denial inasuta nafsi za wengi, hatuwezi kupona

LEO ni siku ya 23 tangu risasi ya kwanza ilipofyatuliwa na kuua vijana waliokuwa...

Watoto mapacha wajinyonga Zanzibar, kisa kazi za ndani

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba linachunguza tukio la kujinyonga kwa...

Yanga yatua Zanzibar kuitengenezea dozi AS FAR Rabat

Na Winfrida Mtoi Kikosi cha Yanga kimetua visiwani Zanzibar kwa maandalizi ya kuikabili AS FAR...

Rais Samia atangaza Baraza Jipya la Mawaziri, nane watemwa

Tatu Mohamed na Winfrida Mtoi RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan,...

More like this

Bado denial inasuta nafsi za wengi, hatuwezi kupona

LEO ni siku ya 23 tangu risasi ya kwanza ilipofyatuliwa na kuua vijana waliokuwa...

Watoto mapacha wajinyonga Zanzibar, kisa kazi za ndani

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba linachunguza tukio la kujinyonga kwa...

Yanga yatua Zanzibar kuitengenezea dozi AS FAR Rabat

Na Winfrida Mtoi Kikosi cha Yanga kimetua visiwani Zanzibar kwa maandalizi ya kuikabili AS FAR...