Biteko aipongeza Ewura kuleta utulivu kwenye nishati

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko, ameipongeza Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), kwa usimamizi thabiti wa huduma za nishati na maji nchini ambao ameeleza kuwa umechangia kuleta na kuimarisha utulivu kwenye sekta ya nishati na taifa kwa ujumla.

Biteko ametoa pongezi hizo juzi wakati akifungua kikao cha nne cha Baraza la Pili la Wafanyakazi wa EWURA kinachofanyika jijini Tanga.

“EWURA mnafanya kazi kubwa ya kudhibiti upatikanaji wa huduma za uhakika za umeme na mafuta nchini kwa ufanisi mkubwa, mmeleta utulivu kwenye sekta ya nishati nchini, mmerahisiha mazingira ya uwekezaji kwenye CNG, vituo vya mafuta vijijini na kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji kwenye nishati safi ya kupikia, nawapongeza sana,” amesema Biteko.

Dkt Biteko amesisitiza EWURA kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, kuendelea kuweka mazingira wezeshi ya kiudhibiti kuhusu ajenda ya misheni 300 ya umeme na kuwasimamia watoa huduma wanaodhibitiwa kuhakikisha wanakuwa na mikataba ya huduma kwa mteja inayotekelezeka.

Aidha, aliitaka EWURA kuhakikisha inaendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara ya mafuta nchini, na kushirikisha wadau na watoa huduma wanaodhibitiwa kwenye maamuzi ya kiudhibiti ili utekelezaji wake uwe na tija.

Katika hatua nyingine, ametoa rai kwa EWURA kufanya tafiti za kina kuhusu huduma zinazodhibitiwa ili kubaini maeneo yanayohitaji kutiliwa mkazo, kufanya kazi kwa weledi na kufuata sheria ikiwamo kupokea hoja za wanaokosoa utendaji wa taasisi ili kuisaidia kujitathmini na kuboresha zaidi utendaji wake.

spot_img

Latest articles

MKURUGENZI BOT AVUTIWA NA UFANISI WA UTUNZAJI KUMBUKUMBU KIDIJITALI WA PSSSF

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Tafiti na Uchumi Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt....

MKANDARASI AKAMILISHA AWAMU YA KWANZA YA UVUTAJI WA NYAYA KATIKA MRADI WA CHALINZE–DODOMA

📌TANESCO yawashukuru wateja kwa uvumilivu na kutangaza awamu ya pili kuanza Agosti 11–14 katika...

Msajili wa Hazina akutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa EADB

Na Mwandishi wa OTR MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, leo, Agosti 4, 2026, amekutana na...

Polisi Rufiji wahamasisha vijana kujikita katika shughuli halali za kiuchumi

Na Mwandishi Wetu, Rufiji JESHI la Polisi Mkoa wa Kipolisi Rufiji limewahimiza vijana kujikita katika...

More like this

MKURUGENZI BOT AVUTIWA NA UFANISI WA UTUNZAJI KUMBUKUMBU KIDIJITALI WA PSSSF

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Tafiti na Uchumi Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt....

MKANDARASI AKAMILISHA AWAMU YA KWANZA YA UVUTAJI WA NYAYA KATIKA MRADI WA CHALINZE–DODOMA

📌TANESCO yawashukuru wateja kwa uvumilivu na kutangaza awamu ya pili kuanza Agosti 11–14 katika...

Msajili wa Hazina akutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa EADB

Na Mwandishi wa OTR MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, leo, Agosti 4, 2026, amekutana na...