Rais wa Malawi aagiza kuondoa majeshi yake DRC

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Malawi, Lazarus Chakwera amemuagiza Kamanda wa Jeshi la nchi hiyo kujiandaa kuondoa Majeshi ya Malawi, kutoka eneo la Mashariki la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kulingana na taarifa Televisheni ya Serikali.

Taarifa hiyo ilisema uamuzi wa Rais unalenga kuheshimu tangazo la kusitisha mapigano kati ya pande zinazozana, ingawa uamuzi wa kusitisha mapigano ulikuwa ni mpango wa waasi wa M23, ambao uliibuka baada ya kundi hilo kushambulia Nyabibwe katika Jimbo la Kivu Kusini mwa DRC.

Rais Lazarus Chakwera alikuwa chini ya shinikizo la kuondoa Majeshi ya nchi yake Mashariki mwa DRC, baada ya wanajeshi watatu wa Malawi kuuawa katika mashambulizi ya M23 mjini Goma.

Wanajeshi hao walikuwa sehemu ya Ujumbe wa kulinda amani wa Kusini mwa Afrika uliotumwa na SADC kusaidia mamlaka ya Congo, kukabiliana na makundi yenye silaha katika eneo la mashariki linalokabiliwa na mzozo.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...