Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi

WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa kikosi hicho Laurindo Aurelio maarufu Depu akitupia bao moja katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo Januari 19,2025 kwenye dimba la KMC Complex, jijini Dar es Salaam.

Depu raia wa Angola ni usajili mpya ndani ya kikosi cha Wananchi ambapo ameonekana kuanza vizuri kwani aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Maxi Nzengeli lakini alifanyikiwa  kufunga na kutoa pasi ya  bao.

Wachezaji wengine waliofunga katika mchezo huo ni Mohammed Damaro, Duke Abuya, Pacome Zouzoua, Prince Dube na Mudathir Yahya.

Matokeo hayo yameifanya Yanga kufikisha pointi 19 na kuongoza msimamo wa Ligi Kuu, ikiwa imecheza michezo saba ikishinda sita na kutoka sare mmoja, huku Mashujaa ikibaki nafasi ya tano na pointi 13 baada ya michezo 10.

Baada mchezo huo Wanajangwani hao wanajiandaa na mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi ambapo wanatarajiwa kukutana na Al Ahly  nchini Misri, Ijumaa Januari 23,2025.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...