WHO yatangaza tarehe ya uchaguzi wa kupatikana mrithi wa Ndugulile

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa Mkurugenzi mpya wa Kanda ya Afrika atachaguliwa Mei mwaka huu.

Uteuzi huo unakuja kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi mteule wa WHO Kanda ya Afrika, Dkt. Faustine Ndugulile aliyefariki dunia Novemba 27, 2024 nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu.

Kutokana na kifo chake, WHO imeamua Mataifa yateue tena wagombea, huku tarehe ya mwisho ya kutuma maombi ikiwa Februari 28, mwaka huu.

Dkt. Tedros Ghebreyesus ametangaza kuwa mchakato wa kura utafanyika Mei 8, 2025 na jina la kiongozi mpya litapitishwa rasmi Agosti 2025.

Aidha WHO imemteua Dkt. Chikwe Ihekweazu kama Kaimu Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika.

spot_img

Latest articles

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

More like this

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...