WHO yatangaza tarehe ya uchaguzi wa kupatikana mrithi wa Ndugulile

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa Mkurugenzi mpya wa Kanda ya Afrika atachaguliwa Mei mwaka huu.

Uteuzi huo unakuja kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi mteule wa WHO Kanda ya Afrika, Dkt. Faustine Ndugulile aliyefariki dunia Novemba 27, 2024 nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu.

Kutokana na kifo chake, WHO imeamua Mataifa yateue tena wagombea, huku tarehe ya mwisho ya kutuma maombi ikiwa Februari 28, mwaka huu.

Dkt. Tedros Ghebreyesus ametangaza kuwa mchakato wa kura utafanyika Mei 8, 2025 na jina la kiongozi mpya litapitishwa rasmi Agosti 2025.

Aidha WHO imemteua Dkt. Chikwe Ihekweazu kama Kaimu Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

More like this

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...