Trump: Sina uhakika na uwepo wa amani Israel na Hamas

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema hana uhakika na kuwepo kwa amani ya kudumu kati ya Israel na Hamas licha ya kuwa sehemu ya mpango wa kusitisha mapigano uliowezesha kuachiwa kwa mateka ambapo akizungumza kabla ya mkutano wake na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, Trump amekiri kuwa hali bado ni tete na haitabiriki.

Netanyahu aliyewasili Washington kwa mazungumzo hayo anakabiliwa na shinikizo kali kutoka kwa washirika wake wenye msimamo mkali wa kisiasa ambao wanataka mashambulizi dhidi ya Hamas yaendelezwe lakini Wakati huo huo Wananchi wa Israel wanamtaka ahakikishe mateka waliosalia wanaachiwa na vita vya miezi 15 vinakoma.

Hata hivyo, Hamas imesisitiza kuwa haitatoa mateka zaidi bila Israel kuondoa Wanajeshi wake kutoka Gaza suala linalozua mgawanyiko ndani ya Serikali ya Netanyahu ambapo Bezalel Smotrich Mshirika wake wa siasa kali ametishia kuiangusha Serikali ikiwa vita dhidi ya Hamas havitaendelea.

Pamoja na hayo, Trump ameibua mpango wa kuwahamisha Wapalestina kutoka Gaza kwenda Misri na Jordan ingawa mataifa hayo yamekataa wazo hilo na Wachambuzi wanaonya kuwa msimamo huo wa Trump unaweza kuhatarisha juhudi za kufanikisha usuluhishi kati ya Israel na Saudi Arabia kwani mazungumzo hayo yanasisitiza kuwa suluhisho pekee ni kuundwa kwa Taifa huru la Palestina.

spot_img

Latest articles

MINZIRO NA PAMBA YAKE NAWAPIGA TU

Na Mwandishi Wetu Timu ya Pamba Jiji chini ya Kocha Felix Minziro (Majeshi, Baba Isaya)...

Majaliwa azitaka Mamlaka za Mikoa, Taasisi za Elimu kusimamia utekelezaji Sera ya elimu

Na Mwandishi Wetu WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amezielekeza mamlaka za mikoa, halmashauri na taasisi za...

Bidhaa ‘feki’ zadidimiza Watanzania lindi la umasikini

Watanzania wanazidi kunasa katika mzunguko wa umasikini unaosababishwa na kushamiri kwa bidhaa duni na...

More like this

MINZIRO NA PAMBA YAKE NAWAPIGA TU

Na Mwandishi Wetu Timu ya Pamba Jiji chini ya Kocha Felix Minziro (Majeshi, Baba Isaya)...

Majaliwa azitaka Mamlaka za Mikoa, Taasisi za Elimu kusimamia utekelezaji Sera ya elimu

Na Mwandishi Wetu WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amezielekeza mamlaka za mikoa, halmashauri na taasisi za...