Gates Foundation yaipongeza Tanzania uboreshaji afya ya msingi na kupunguza vifo vya kina mama na watoto

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepongezwa kutokana na jitihada madhubuti za kuimarisha afya ya msingi na kupunguza idadi ya vifo vya kina mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano.

Pongezi hizo zimetolewa leo Januari 31, mwaka huu na Mkurugenzi Mkuu wa Gates Foundation Barani Afrika, Dkt. Paulin Basinga alipotembelea Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambapo alipata fursa ya kuona jinsi inavyotoa mchango wake kwa Serikali kuimarisha upatikanaji huduma ngazi ya afya ya msingi, hospitali za rufaa za mikoa hadi Kanda na hatimaye kupunguza rufaa za wagonjwa kufika hospitalini hapo ikiwemo kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda nje ya nchi.

Dkt. Basinga amesema taasisi anayoiongoza imefanya kazi na Serikali ya Tanzania katika maeneo ya uboreshaji programu za kilimo, masuala ya fedha kwa ujumla wake, sekta ya afya hususani kufanya tafiti zilizoibua afua mbalimbali za kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano.

Katika hatua nyingine, Dkt. Basinga ameipongeza MNH ambayo ni hospitali ngazi ya juu ya nne nchini kutokana na huduma za ubingwa na ubingwa bobezi inazotoa kwa wananchi wa ndani, mataifa jirani, mazingira bora ya utoaji huduma na utayari wa watoa huduma kuhudumia wananchi katika hospitali hiyo.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Prof. Mohamed Janabi amemshukuru Dkt. Basinga kutembelea hospitali hiyo na kumhakikishia kuwa hospitali hiyo kwa nafasi yake inafanya kazi kubwa kwa niaba ya Serikali katika kuimarisha huduma nchini ikiwemo huduma ngazi ya msingi hadi ngazi ya kanda.

Prof. Janabi ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kutokana na jitihada za kuongeza idadi ya zahanati, vituo vya afya, hospitali za wilaya na wahudumu wa afya ngazi ya jamii ili kuimarisha huduma katika maeneo hayo na kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto wachanga chini ya miaka mitano.

spot_img

Latest articles

WATAHINIWA 1.16 MILIONI KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 1,168,649 kutoka shule 20,019 Tanzania Bara wanatarajiwa...

TANESCO YATUNUKIWA TUZO KUTAMBUA MCHANGO WA UBUNIFU NA MAENDELEO YA NISHATI

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limekabidhiwa tuzo ya kwa kutambua mchango...

TANESCO YABORESHA MAISHA YA WAFANYAKAZI NYUMBA YA MUNGU

📌 Nyumba za wafanyakazi zakarabatiwa, kuboresha utendaji wa kazi 📌 Mtambo wa kisasa wa kuchakata...

KATAMBI ATOA ONYO KWA MAKUNDI YA ULINZI YASIYO RASMI

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, ametoa onyo kwa...

More like this

WATAHINIWA 1.16 MILIONI KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 1,168,649 kutoka shule 20,019 Tanzania Bara wanatarajiwa...

TANESCO YATUNUKIWA TUZO KUTAMBUA MCHANGO WA UBUNIFU NA MAENDELEO YA NISHATI

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limekabidhiwa tuzo ya kwa kutambua mchango...

TANESCO YABORESHA MAISHA YA WAFANYAKAZI NYUMBA YA MUNGU

📌 Nyumba za wafanyakazi zakarabatiwa, kuboresha utendaji wa kazi 📌 Mtambo wa kisasa wa kuchakata...