TANZANIA YAWEKA REKODI MKUTANO WA WAHASIBU WAKUU AFRIKA

Na Mwandishi Wetu

Tanzania imeweka rekodi ya Mkutano wa Pili wa Wahasibu Wakuu wa Serikali Barani Afrika kwa kuwa na washiriki zaidi ya 2000 kutoka ndani na nje ya Bara la Afrika ikiwa ni idadi kubwa kuwahi kufikiwa tangu kuanzishwa kwa Jumuiya ya Wahasibu Wakuu wa Serikali Afrika.

Mkutano huo ulioanza  Desemba 2, 2024, ukibeba kauli mbiu ya “Kujenga Imani ya Umma katika Mifumo ya Usimamizi wa Fedha za Umma kwa Ukuaji Endelevu” uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AIC), umepokelewa kipekee huku ukikusanya Wahasibu, Wakaguzi wa Ndani na Wataalam wa kada zenye uhusiano wa karibu na uhasibu kama; Wakaguzi wa Hesabu, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA.

Aidha kupitia mkutano huo, washiriki walipata fursa ya kupata ufahamu kutoka kwa wataalam  wa sekta ya umma kuhusu mwelekeo wa kisasa, changamoto, na ubunifu katika usimamizi wa fedha za umma.

Mada mbalimbali zilijadiliwa, kuanzia mabadiliko ya kidijitali katika ufanisi wa sekta ya umma hadi kupambana na mtiririko haramu wa fedha, huku ikitolewa fursa bora za kujifunza ambazo zinaweza kutumika moja kwa moja katika majukumu ya kila siku ya wahasibu na wataalamu wa fedha.


Akizungumza wakati wa Kufunga Mkutano huo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko, aliwaasa wahasibu kusimamia taaluma yao kwa kuzingatia misingi ya kitaaluma, na kujiongezea ujuzi ili kuendana na mabadiliko ya
teknolojia.

“Nataka niwaombe wahasibu mtambue kuwa taaluma yenu ni muhimu hata chochote kinachotokea katika sehemu zenu za kazi mtalaumia, hivyo mzuie hasara zinazoweza kutokea” amesema Dkt. Biteko.

Naye Naibu Waziri wa Fedha,  Hamad Hassan Chande, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha,  Dk. Mwigulu Nchemba, aliwataka wahasibu wote Barani Afrika, kuwa waaminifu na kuzisaidia nchi zao katika kuhakikisha zinapata maendeleo.

Alisema kuwa kazi zozote zinazofanywa hususani za miradi ya maendeleo katika nchi za Bara la Afrika zinawahusisha wahasibu hivyo, wazingatie maadili ya taaluma zao na miongozo inayotolewa katika nchi zao ili kuhakikisha malengo yanayopangwa yanafanikiwa.

spot_img

Latest articles

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

Na Mwandishi Wetu, Mwanza MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung...

More like this

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...