Balozi Nchimbi awafariji Mzee Makamba na Familia ya Mwambi

Na Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amemtembelea na kuzungumza na Mzee Yusuf Makamba leo, tarehe 25 Oktoba 2024, jijini Dar es Salaam.

Balozi Nchimbi alifika nyumbani kwa Mzee Makamba, eneo la Wazo Hill, kumfariji kufuatia msiba wa mtoto wake, Sakida Rajab Yusuf Makamba, aliyefariki dunia tarehe 12 Oktoba 2024, mjini Morogoro.

Mzee Makamba, ambaye pia ni Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM, alimshukuru Balozi Nchimbi kwa kufika kumpatia pole na alitumia fursa hiyo kumpongeza pamoja na Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) kwa juhudi zao katika kuimarisha chama.

“Sisi tunawaona, tunawasikia, na tunawafuatilia. Endeleeni kuijenga na kuimarisha CCM. WanaCCM waendelee kufanya kazi ya kujenga na kuimarisha chama kwa bidii zote. Hakuna mwingine atakayefanya kazi hiyo bali wanaCCM wenyewe,” alisema Mzee Makamba.

Mapema kabla, Balozi Nchimbi, akiwa ameambatana na  Issa Gavu, Katibu wa NEC ya CCM Taifa – Oganaizesheni, alifika pia kuifariji familia ya marehemu Balozi Jaka Mwambi, aliyewahi kuwa Naibu Katibu Mkuu, kufuatia msiba wa mtoto wake, Happiness Jaka Mwambi, aliyefariki dunia Oktoba 24,2024, jijini Dar es Salaam.

spot_img

Latest articles

Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili...

Waziri Aweso aweka kambi Dar kupambana na changamoto upungufu wa maji

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso (Mb) amefanya ziara ya kikazi katika...

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

More like this

Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili...

Waziri Aweso aweka kambi Dar kupambana na changamoto upungufu wa maji

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso (Mb) amefanya ziara ya kikazi katika...

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...