Milioni 300 zawekezwa kiwanda cha YLM Food Company Limited

Na Grace Mwakalinga

SHILINGI milioni 300 zimetumika kuwekeza kiwanda cha YLM Food Company Limited kilichopo Kiwalani jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuzalisha karanga za YY ambazo tayari zimeingizwa sokoni.

Kwa mujibu wa Meneja wa kiwanda hicho, Christopher Godfrey, amesema hadi sasa wamezalisha ajira zaidi 20 na kwamba wanaendelea kufungua fursa za ajira kupitia bidhaa hizo za karanga ambazo tayari zimewekwa sokoni.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho , Mi Yuiing amemtangaza, muigizaji maarufu nchini, Shamsha Ford kuwa balozi wa bidhaa za Karanga za YY na kwamba wana imani na msanii huyo kutangaza bidhaa hizo nchini.

Aidha Yuiing ameeleza kufahishwa na mazingira mazuri ya uwekezaji nchini ambayo yamemvutia kuwekeza sambamba na ziara za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan nchini China kuitangaza Tanzania katika fursa za kibiashara.

“Uwekezaji huu sio tu kwa ajili ya uzalishaji wa karanga, bali pia unatoa nafasi za ajira kwa vijana zaidi na tunatarajia kutoa fursa zaidi kwa watu hususani wanaohitaji uwakala wa bidhaa za karanga za YY,” alisema Yuiing.

Balozi wa YY Karanga, Shamsa Ford, amewataka wafanyabiashara na mawakala kuchangamkia fursa ya bidhaa hizo ili kujiingizia kipato na amewahakikishia wananchi kuhusu ubora wa bidhaa zinazozalishwa na kiwanda hicho.

“Kiwanda hiki kinatoa fursa kwa watanzania kujiajiri, kupata ajira, na kukuza uchumi kwa wale wanaotafuta fursa za biashara, uwekezaji huu ni hatua nzuri ya kuweza kuuza na kusambaza karanga,” amesema Shamsha.

spot_img

Latest articles

TAEC YAFANYA UKAGUZI WA MATUMIZI SALAMA YA MIONZI MKOANI LINDI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bwn. Natalis Linuma, amesema...

Msajili wa Hazina aitaka TANROADS kuongeza ufanisi

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, leo, Septemba 18, 2026, ametoa...

TANESCO IMEJIPANGA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO – MD TWANGE

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema limejipanga kukabiliana na...

MRADI WA UMEME SIMIYU KUFUNGUA FURSA ZA UWEKEZAJI NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI WANANCHI

📌 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mhe.Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba...

More like this

TAEC YAFANYA UKAGUZI WA MATUMIZI SALAMA YA MIONZI MKOANI LINDI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bwn. Natalis Linuma, amesema...

Msajili wa Hazina aitaka TANROADS kuongeza ufanisi

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, leo, Septemba 18, 2026, ametoa...

TANESCO IMEJIPANGA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO – MD TWANGE

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema limejipanga kukabiliana na...