Milioni 300 zawekezwa kiwanda cha YLM Food Company Limited

Na Grace Mwakalinga

SHILINGI milioni 300 zimetumika kuwekeza kiwanda cha YLM Food Company Limited kilichopo Kiwalani jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuzalisha karanga za YY ambazo tayari zimeingizwa sokoni.

Kwa mujibu wa Meneja wa kiwanda hicho, Christopher Godfrey, amesema hadi sasa wamezalisha ajira zaidi 20 na kwamba wanaendelea kufungua fursa za ajira kupitia bidhaa hizo za karanga ambazo tayari zimewekwa sokoni.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho , Mi Yuiing amemtangaza, muigizaji maarufu nchini, Shamsha Ford kuwa balozi wa bidhaa za Karanga za YY na kwamba wana imani na msanii huyo kutangaza bidhaa hizo nchini.

Aidha Yuiing ameeleza kufahishwa na mazingira mazuri ya uwekezaji nchini ambayo yamemvutia kuwekeza sambamba na ziara za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan nchini China kuitangaza Tanzania katika fursa za kibiashara.

“Uwekezaji huu sio tu kwa ajili ya uzalishaji wa karanga, bali pia unatoa nafasi za ajira kwa vijana zaidi na tunatarajia kutoa fursa zaidi kwa watu hususani wanaohitaji uwakala wa bidhaa za karanga za YY,” alisema Yuiing.

Balozi wa YY Karanga, Shamsa Ford, amewataka wafanyabiashara na mawakala kuchangamkia fursa ya bidhaa hizo ili kujiingizia kipato na amewahakikishia wananchi kuhusu ubora wa bidhaa zinazozalishwa na kiwanda hicho.

“Kiwanda hiki kinatoa fursa kwa watanzania kujiajiri, kupata ajira, na kukuza uchumi kwa wale wanaotafuta fursa za biashara, uwekezaji huu ni hatua nzuri ya kuweza kuuza na kusambaza karanga,” amesema Shamsha.

spot_img

Latest articles

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

More like this

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...