Jay Melody kutoana jasho na Diamond, Alikiba

Na Winfrida Mtoi

Kamati ya Tuzo  za Muziki Tanzania (TMA) leo Agosti 29,2024 imetangaza wanaowania tuzo za muziki  nchini, wakianza  na vipengele vitatu ambavyo ni ni Mwanamuziki bora wa kiume wa mwaka, wimbo bora wa taarabu wa mwaka na wimbo bora Afrika Mashariki, Kusini na Magharibi.

Katika kipengele cha Msanii Bora wa Kiume wa mwaka, wanaowania ni Marioo kupitia wimbo ‘Shisha’, Diamond Platnumz ‘Shuu’, Harmonize ‘Single Again’, Alikiba ‘Sumu’ na Jay Melody wimbo wa ‘Nitasema’.

Vipengele vingine vilivyotangazwa  ni wimbo bora wa taarabu wa mwaka ambapo kuna  wimbo wa ‘Watu na Viatu’ wa  Malkia Layla Rashid, ‘Hatuachani’ ya Amina Kidevu, ‘Bila Yeye Sijiwezi’ ya Mwinyi ‘Mkuu, Sina Wema’ ya Mwasiti Mbwana na ‘DSM Sweetheart’ ya Salha.

Wimbo bora Afrika Mashariki, Kusini na Magharibi kuna ‘People’ ya Libianca, ‘American Love’ ya Qing Madi, ‘Lonely at the Top’ ya Asake, ‘Unavailable’ ya Davido ft Musa Keys na ‘Mnike’ ya Tyler ICU.

Kamati ya Tuzo inayoongozwa na Mwenyekiti wake David Minja na Makamu Mwenyekiti Seven Mosha wamesema vipengele vingine vitaendelea kutangazwa, huku mashabiki wakitakiwa kujindaa kuwapigia kura wasanii wao wanaowapenda kuanzia Septemba 3,2024.

spot_img

Latest articles

VETA yajivunia mageuzi makubwa, yazidi kuwanufaisha Watanzania

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imesema inajivunia mafanikio...

TPDC yapata Tuzo ya Taasisi Bora Sabasaba kwa miaka mitano mfululizo

Na Tatu Mohamed SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeandika historia kwa kutwaa tuzo...

Rais Mwinyi atembelea Banda la ETDCO Sabasaba

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein...

GF Trucks yaibuka mshindi wa jumla maonesho ya Sabasaba 2025

Na Mwandishi Wetu Kampuni ya Gf Trucks & Equipment imeibuka mshindi wa jumla katika Maonesho...

More like this

VETA yajivunia mageuzi makubwa, yazidi kuwanufaisha Watanzania

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imesema inajivunia mafanikio...

TPDC yapata Tuzo ya Taasisi Bora Sabasaba kwa miaka mitano mfululizo

Na Tatu Mohamed SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeandika historia kwa kutwaa tuzo...

Rais Mwinyi atembelea Banda la ETDCO Sabasaba

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein...