GF Trucks yaibuka mshindi wa jumla maonesho ya Sabasaba 2025

Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya Gf Trucks & Equipment imeibuka mshindi wa jumla katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba 2025 , kupitia kiwanda chake cha kuunganisha magari makubwa cha GF Vehicle Assemblers(GFA) kilichopo Kibaha mkoani Pwani

Katika maonesho hayo yanayoendelea jijini Dar es Salaam, yameshirikisha makampuni na wafanyabiashara mbambali wa ndani ya chini na nje kama vile China, Korea, Uturuki , Ulaya na Afrika.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Hussen Ali Mwinyi alizindua maonesho hayo jana Julai 7,2025 ambapo alitembelea baadhi ya mabanda kabla ya kuanza kutoa tuzo na zawadi kwa washindi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Hussein Mwinyi akimsikiliza Mkurugenzi wa GF, Ali Karmal wakati alipotembelea banda la kampuni hiyo kwenye maonyesho ya Sabasaba.

Miongonj mwa mabanda aliyotembelea ni Rais Mwinyi nj la GF na kujionea bidhaaa mbalimbali zinazouzwa na kampuni hiyo ambazo magari madogo ya Hyundai, Mahindra, magari makubwa aina ya FAW , mashine na mitambo ya XCMG.

Pia alijionea jinsi michakato ya awali ya uunganishaji wa magari unavyofanyika kupitia kiwanda cha kampuni hiyo.

Akizungumza wakati wa kutoa tuzo hiyo, Rais Mwinyi aliwapongeza GF kwa kuibuka kuwa vinara wa maonyesho hayo na kuwataka wasibweteke na kupanua zaidi katika uwekezaji, huku akiwakaribisha Zanzibar.

Naye Mkurugezi wa kampuni ya GF ,Ali Karmali amesema wanajivuni kuwekeza nchini kama kiwanda cha kwanza cha kutengeneza magari ya aina zote kutokana na mazingira mazuri yaliyowekwa na Serikali kwa wawekezaji.

“Tunajivunia kuwa waongoza njia na makampuni mengine yajifunze kwetu kupitia kiwanda chetu cha kuunganisha magari na tupo katika awamu ya tatu ya upanuzi itakayochukua zaidi ya wafanyakazi 3000 hivo kuongeza ajira kwa watanzania,” amesema.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...