Jay Melody kutoana jasho na Diamond, Alikiba

Na Winfrida Mtoi

Kamati ya Tuzo  za Muziki Tanzania (TMA) leo Agosti 29,2024 imetangaza wanaowania tuzo za muziki  nchini, wakianza  na vipengele vitatu ambavyo ni ni Mwanamuziki bora wa kiume wa mwaka, wimbo bora wa taarabu wa mwaka na wimbo bora Afrika Mashariki, Kusini na Magharibi.

Katika kipengele cha Msanii Bora wa Kiume wa mwaka, wanaowania ni Marioo kupitia wimbo ‘Shisha’, Diamond Platnumz ‘Shuu’, Harmonize ‘Single Again’, Alikiba ‘Sumu’ na Jay Melody wimbo wa ‘Nitasema’.

Vipengele vingine vilivyotangazwa  ni wimbo bora wa taarabu wa mwaka ambapo kuna  wimbo wa ‘Watu na Viatu’ wa  Malkia Layla Rashid, ‘Hatuachani’ ya Amina Kidevu, ‘Bila Yeye Sijiwezi’ ya Mwinyi ‘Mkuu, Sina Wema’ ya Mwasiti Mbwana na ‘DSM Sweetheart’ ya Salha.

Wimbo bora Afrika Mashariki, Kusini na Magharibi kuna ‘People’ ya Libianca, ‘American Love’ ya Qing Madi, ‘Lonely at the Top’ ya Asake, ‘Unavailable’ ya Davido ft Musa Keys na ‘Mnike’ ya Tyler ICU.

Kamati ya Tuzo inayoongozwa na Mwenyekiti wake David Minja na Makamu Mwenyekiti Seven Mosha wamesema vipengele vingine vitaendelea kutangazwa, huku mashabiki wakitakiwa kujindaa kuwapigia kura wasanii wao wanaowapenda kuanzia Septemba 3,2024.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...