Jay Melody kutoana jasho na Diamond, Alikiba

Na Winfrida Mtoi

Kamati ya Tuzo  za Muziki Tanzania (TMA) leo Agosti 29,2024 imetangaza wanaowania tuzo za muziki  nchini, wakianza  na vipengele vitatu ambavyo ni ni Mwanamuziki bora wa kiume wa mwaka, wimbo bora wa taarabu wa mwaka na wimbo bora Afrika Mashariki, Kusini na Magharibi.

Katika kipengele cha Msanii Bora wa Kiume wa mwaka, wanaowania ni Marioo kupitia wimbo ‘Shisha’, Diamond Platnumz ‘Shuu’, Harmonize ‘Single Again’, Alikiba ‘Sumu’ na Jay Melody wimbo wa ‘Nitasema’.

Vipengele vingine vilivyotangazwa  ni wimbo bora wa taarabu wa mwaka ambapo kuna  wimbo wa ‘Watu na Viatu’ wa  Malkia Layla Rashid, ‘Hatuachani’ ya Amina Kidevu, ‘Bila Yeye Sijiwezi’ ya Mwinyi ‘Mkuu, Sina Wema’ ya Mwasiti Mbwana na ‘DSM Sweetheart’ ya Salha.

Wimbo bora Afrika Mashariki, Kusini na Magharibi kuna ‘People’ ya Libianca, ‘American Love’ ya Qing Madi, ‘Lonely at the Top’ ya Asake, ‘Unavailable’ ya Davido ft Musa Keys na ‘Mnike’ ya Tyler ICU.

Kamati ya Tuzo inayoongozwa na Mwenyekiti wake David Minja na Makamu Mwenyekiti Seven Mosha wamesema vipengele vingine vitaendelea kutangazwa, huku mashabiki wakitakiwa kujindaa kuwapigia kura wasanii wao wanaowapenda kuanzia Septemba 3,2024.

spot_img

Latest articles

Haikubaliki, hali hii ya D’Salaam inachefua

KATIKA siku za hivi karibuni kumekuwa na matamko ya operesheni mbalimbali za kurejesha uzingatiaji...

Mwanasheria Mkuu asisitiza mageuzi ya Sheria za Anga

Na Mwandishi Wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesisitiza juu ya umuhimu wa...

Wananchi Peramiho, Shiwinga kupiga Kura kesho kuchagua Mbunge, Diwani

Na Mwandishi Wetu WAPIGA Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura...

MIF 2026 kujadili mikakati ya kufikia uchumi wa kati wa juu 2050

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imesema Mkutano wa Jukwaa la Wakurugenzi wa Bodi na Watendaji...

More like this

Haikubaliki, hali hii ya D’Salaam inachefua

KATIKA siku za hivi karibuni kumekuwa na matamko ya operesheni mbalimbali za kurejesha uzingatiaji...

Mwanasheria Mkuu asisitiza mageuzi ya Sheria za Anga

Na Mwandishi Wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesisitiza juu ya umuhimu wa...

Wananchi Peramiho, Shiwinga kupiga Kura kesho kuchagua Mbunge, Diwani

Na Mwandishi Wetu WAPIGA Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura...