Tanzania, Morocco katika jukwaa la biashara

NA GRACE MWAKALINGA

SERIKALI ya Morocco imeandaa Jukwaa la Biashara na Tanzania kwa lengo la kujenga na kukuza ushirikiano wa biashara, pamoja na kufungua fursa katika sekta za kilimo, utalii, miundombinu, nishati mbadala, usimamizi wa bandari na teknolojia.

Balozi wa Ufalme wa Morocco nchini, Zakaria El Goumiri amesema ushirikiano wa nchi hizo mbili ukuza biashara baina ya nchi hizo mbili na kwamba takwimu zinaonesha ukuaji kutoka dola milioni 28 mwaka 2016 hadi dola milioni 285.5 mwaka 2022.

Balozi El Goumiri alikuwa akizungumza kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 25 tangu kutawazwa Mfalme Mohammed wa VI wa Morocco.

“Serikali zetu zimekubaliana kuandaa awamu ya pili ya Jukwaa la Biashara la Morocco na Tanzania baadaye mwaka huu, dhumuni litakuwa ni kubaini fursa mpya za uwekezaji, kujenga ushirikiano thabiti, na kuendeleza maendeleo ya nchi zetu mbili,” El Goumiri.

Kwa upande wake Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Pindi Chana amesema maadhimisho ya Miaka 25 ya kuwekwa Madarakani kwa Mtukufu Mfalme Mohammed VI ni fursa nzuri ya kutafakari juu ya mafanikio ambayo Ufalme wa Morocco umeyapata tangu tarehe Julai 30, 1999.

Dk. Chana anasema Ufalme huo umekuwa ukitoa misaada ambayo inajumuisha utoaji wa zaidi ya nafasi za masomo 8,000 kwa nchi kadhaa za Afrika, ikiwemo Tanzania.

“Tanzania na Morocco zina uhusiano wa muda mrefu ambao ulianza hata kabla ya ukoloni ambapo watu wetu walikuwa wakishirikiana kwa karibu kupitia biashara na shughuli nyingine za kijamii na kitamaduni,” anasema Waziri Chana na kuongeza:

“Ushirikiano umezidi kuimarika baada ya ziara ya Kiserikali ya Mtukufu Mfalme nchini Tanzania mnamo Oktoba 2016 na wakati wa ziara hiyo, mikataba 22 ilisainiwa katika maeneo mbalimbali ya ushirikiano, ikiwa ni pamoja na ulinzi na usalama, biashara na uwekezaji, kilimo, utalii, usafiri, afya, elimu, utamaduni, na michezo,” amesema Dk. Balozi Pindi Chana.

spot_img

Latest articles

Simba yapewa wakusanya kodi, Yanga maafande

Na Mwandishi Wetu DROO ya hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho,...

Waziri Mkuu ahimiza ufungaji kamera  viwanjani kudhibiti ushirikina

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk.Mwigulu Nchemba, amehimiza ufungaji wa kamera nyingi katika viwanja vya...

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

More like this

Simba yapewa wakusanya kodi, Yanga maafande

Na Mwandishi Wetu DROO ya hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho,...

Waziri Mkuu ahimiza ufungaji kamera  viwanjani kudhibiti ushirikina

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk.Mwigulu Nchemba, amehimiza ufungaji wa kamera nyingi katika viwanja vya...

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...