Watu wawili wafariki, 16 wajeruhiwa katika ajali ya basi Songwe

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Watu wawili wamefariki dunia na wengine 16 kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugonga daraja na kutumbukia mtoni katika eneo la Mlima Myovizi, mkoani Songwe.

Ajali hiyo, iliyotokea leo Julai 15 saa 12 asubuhi, ilihusisha basi la Ngasere High Class lililokuwa likisafiri kutoka Dodoma kwenda Tunduma, mkoani Songwe.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe, Gallus Hyera, amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo viwili na majeruhi 16 katika ajali hiyo, ambayo ilitokea baada ya basi hilo kugonga nguzo ya daraja na kutumbukia mtoni.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbozi, Dk. Kelvin Masae, amethibitisha kupokea majeruhi 16 ambao wanaendelea kupatiwa matibabu, huku wengine wakipewa rufaa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...