Waziri Kairuki aipongeza Tawa usimamizi rasilimali za wanyamapori

Na Joyce Ndunguru, Morogoro

Waziri wa Maliasili na Utalii, Angellah Kairuki ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kwa usimamizi mzuri wa rasilimali za wanyamapori.

Kairuki ametoa pongezi hizo leo Julai 8,2024 wakati wa ziara yake ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo mkoani Morogoro kwa lengo la kusikiliza changamoto na kutoa utatuzi ili kuboresha utendaji kazi wa mamlaka hiyo.

“Nawapongeza TAWA kwa usimamizi mzuri wa rasilimali za wanyamapori kwa kuzingatia kuwa ni taasisi ambayo haina muda mrefu tangu kuanzishwa kwake,” amesema Kairuki.

Katika ziara hiyo Kairuki alipata fursa ya kuzungumza na watumishi wa TAWA na kusisitiza kuhusu uzingatiaji wa sheria, kanuni, miongozo na taratibu katika kutimiza majukumu yao ili kuboresha utendaji kazi.

Kuhusu changamoto ya wanyama wakali na waharibifu iliyowasilishwa na Menejimenti, Kairuki alielekeza miradi ya ujirani mwema ijikite katika kutatua changamoto hiyo kama vile ujengaji wa vizimba pamoja na utoaji wa vitendea kazi kama pikipiki ili kuzipunguza.

Kwa upande wake, Kamishna wa Uhifadhi TAWA, Mabula Nyanda, alimshukuru, Waziri Kairuki kwa kuitembelea mamlaka hiyo na kuahidi utekelezaji wa maelekezo yote aliyoyatoa.

Awali Kaimu Naibu Kamishna anayeshughulikia huduma za uhifadhi, Mlage Kabange, alitoa taarifa kuhusu maeneo yanayosimamiwa na TAWA huku akibainisha mafanikio na jitihada zinazofanywa katika kupambana na wanyamapori wakali na waharibifu.

Katika ziara hiyo, Waziri Kairuki aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Fortunata Msoffe, Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Wizara ya Maliasili na Utalii, Abdallah Mvungi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Wizara ya Maliasili na Utalii, Lucy Saleko.

spot_img

Latest articles

Dkt Biteko: Serikali kuendelea kuwekeza katika sekta ya Afya

📌 Dkt. Biteko atambelea Hospitali ya Wilaya ya Meru Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeahidi kuendelea...

THRDC yashauri kuitishwa mkutano wa kitaifa wa maridhiano

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC)...

Sh. Bilioni 30 zaidhinishwa kujenga Barabara zilizoathiriwa na mvua

Na Mwandishi Wetu SERIKALI ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imepanga kutumia kiasi cha...

Ewura yazitaka kampuni za gesi kuongeza mawakala, kudhibiti uchakachuaji wa gesi

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za nishati na...

More like this

Dkt Biteko: Serikali kuendelea kuwekeza katika sekta ya Afya

📌 Dkt. Biteko atambelea Hospitali ya Wilaya ya Meru Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeahidi kuendelea...

THRDC yashauri kuitishwa mkutano wa kitaifa wa maridhiano

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC)...

Sh. Bilioni 30 zaidhinishwa kujenga Barabara zilizoathiriwa na mvua

Na Mwandishi Wetu SERIKALI ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imepanga kutumia kiasi cha...