Uhuru atoa wito kwa viongozi kuwasikiliza wananchi

Nairobi, Kenya

Rais wa zamani wa Kenya Uhuru Kenyatta, ametoa wito wa amani kufuatia maandamano ya kupinga Muswada wa Fedha wa 2024 ambayo siku ya Jumanne yalikumbwa na matukio ya vurugu baada ya waandamanaji kuvamia Bunge la Taifa.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, Uhuru alielezea masikitiko yake kuhusu Wakenya waliouawa wakati wa maandamano, akisisitiza umuhimu wa viongozi waliochaguliwa kuwasikiliza waliowapigia kura.

“Wakati huu wa majaribu, nataka kuwakumbusha viongozi wote kwamba walichaguliwa na wananchi. Kuwasikiliza wananchi si chaguo bali ni wajibu uliowekwa katika misingi ya katiba yetu na katika misingi ya demokrasia,” alisema.

Uhuru, aliongeza kuwa serikali haifai kutumia nguvu na kuwa na upinzani dhidi ya Wakenya wanaotekeleza haki zao za kikatiba kwa maandamano ya amani.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

More like this

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...