Rais Ruto akubali yaishe, akataa kutia saini Muswada wa Fedha

Nairobi, Kenya

Rais wa Kenya, William Ruto, amekataa kutia saini na ameondoa kabisa muswada wenye utata wa fedha wa mwaka 2024, ambao umesababisha maandamano na vurugu nchini kote. Rais Ruto ametoa hotuba hiyo leo Juni 26,2024 kwa taifa baada ya maandamano makubwa yaliyofanyika nchini Kenya, hasa yakiongozwa na vijana waliolalamikia nyongeza mpya za ushuru wakisema zitawaongezea mzigo wa maisha.

Taarifa hii imekuja wakati waandamanaji wakiapa kuendelea na maandamano yao kupinga nyongeza hizo za ushuru, siku moja tu baada ya polisi kufyatua risasi na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 20 katika maandamano hayo yaliyogeuka kuwa vurugu.

Spika wa Bunge la Taifa, Moses Wetangula, amewasifu vijana kwa ujasiri wao, lakini amesisitiza kwamba malalamiko yao lazima yafuate mkondo wa sheria ili yapate kusikilizwa.

Katika hali nyingine, mahakama ya Eldoret imesitisha operesheni zake kwa muda baada ya waandamanaji kuharibu hati muhimu hapo jana.

spot_img

Latest articles

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

Na Mwandishi Wetu, Mwanza MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung...

More like this

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...