Rais Ruto akubali yaishe, akataa kutia saini Muswada wa Fedha

Nairobi, Kenya

Rais wa Kenya, William Ruto, amekataa kutia saini na ameondoa kabisa muswada wenye utata wa fedha wa mwaka 2024, ambao umesababisha maandamano na vurugu nchini kote. Rais Ruto ametoa hotuba hiyo leo Juni 26,2024 kwa taifa baada ya maandamano makubwa yaliyofanyika nchini Kenya, hasa yakiongozwa na vijana waliolalamikia nyongeza mpya za ushuru wakisema zitawaongezea mzigo wa maisha.

Taarifa hii imekuja wakati waandamanaji wakiapa kuendelea na maandamano yao kupinga nyongeza hizo za ushuru, siku moja tu baada ya polisi kufyatua risasi na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 20 katika maandamano hayo yaliyogeuka kuwa vurugu.

Spika wa Bunge la Taifa, Moses Wetangula, amewasifu vijana kwa ujasiri wao, lakini amesisitiza kwamba malalamiko yao lazima yafuate mkondo wa sheria ili yapate kusikilizwa.

Katika hali nyingine, mahakama ya Eldoret imesitisha operesheni zake kwa muda baada ya waandamanaji kuharibu hati muhimu hapo jana.

spot_img

Latest articles

Mandonga ampa jina jipya Kaoneka, King Class na Nasibu Ramadhani moto utawaka

Na Mwandishi Wetu Kuelekea pambano la ngumi la 'Dar Boxing Derby', bondia Karim Mandonga kama...

FCC yawahamasisha wananchi kulinda Afya na Haki zao dhidi ya Bidhaa Bandia

Na Tatu Mohamed TUME ya Ushindani (FCC) imewataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika kulinda...

PSPTB yatangaza Mitihani ya 31 ya Kitaaluma, Usajili kufungwa Agosti 15, mwaka huu

Na Tatu Mohamed BODI ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetangaza kuendesha Mitihani ya...

Ewura CCC: Wananchi wadai fidia wanapocheleweshewa kuunganishiwa maji kwa siku saba za kazi

Na Tatu Mohamed BARAZA la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji...

More like this

Mandonga ampa jina jipya Kaoneka, King Class na Nasibu Ramadhani moto utawaka

Na Mwandishi Wetu Kuelekea pambano la ngumi la 'Dar Boxing Derby', bondia Karim Mandonga kama...

FCC yawahamasisha wananchi kulinda Afya na Haki zao dhidi ya Bidhaa Bandia

Na Tatu Mohamed TUME ya Ushindani (FCC) imewataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika kulinda...

PSPTB yatangaza Mitihani ya 31 ya Kitaaluma, Usajili kufungwa Agosti 15, mwaka huu

Na Tatu Mohamed BODI ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetangaza kuendesha Mitihani ya...