Bunge la Kenya laidhinisha kutumiwa kwa Jeshi, Mahakama yaweka ngumu

Nairobi, Kenya

Bunge la Kenya limeidhinisha ombi la Baraza la Ulinzi la kutumiwa kwa Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) kutoa ulinzi kufuatia maandamano ya kupinga Muswada wa Fedha kote nchini. Kulingana na Waraka wa Amri ya Ziada iliyopangwa Jumatano, Juni 26, hatua hiyo itaambatana na Kifungu cha 241 cha Katiba kinachohitaji kuidhinishwa na Bunge kabla ya wanajeshi kutumiwa kushughulikia masuala ya usalama wa ndani.

Hoja hiyo iliwasilishwa Bungeni baada ya ombi kutolewa na Baraza la Ulinzi siku ya Jumatano. “Kwa mujibu wa Kifungu cha 241(3)(c) cha Katiba na vifungu 31(1)(b), 31(1)(c) na 32 vya Sheria ya Majeshi ya Ulinzi ya Kenya, Sura ya 199, Bunge hili linaidhinisha ombi la Baraza la Ulinzi la tarehe 26 Juni 2024 na, kwa maslahi ya usalama wa taifa, IMERIDHIA kutumwa kwa Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) kusaidia Huduma ya Kitaifa ya Polisi katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Kenya yaliyoathiriwa na maandamano ya ghasia yanayoendelea, ambayo yamesababisha uharibifu wa miundombinu muhimu hadi hali ya kawaida irejeshwe,” sehemu ya ilani hiyo ilisema.

Bunge pia limeahirisha vikao vyake vya kawaida hadi Jumanne, Julai 23, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani.

Maandamano hayo, yaliyopewa jina la “Maandamano ya Gen Z,” yamezua ghasia kubwa, ambapo vijana walivamia majengo ya Bunge na kusababisha uharibifu mkubwa na kuchoma sehemu ya bunge hilo.

Mahakama yazuia kutumwa kwa Jeshi

Chama cha Wanasheria nchini Kenya (LSK) kimepata kibali kutoka kwa mahakama kusimamisha serikali kutuma jeshi la KDF kukabiliana na waandamanaji wanaopinga Mswada wa Fedha 2024. Agizo la kutuma jeshi lilichapishwa Jumanne kwenye Gazeti Rasmi la Serikali na kutiwa saini na Waziri wa Ulinzi Aden Duale, na kuzungumziwa na Rais William Ruto kwenye hotuba yake kwa taifa, punde baada ya ghasia kubwa zilizoshuhudiwa na zilizopelekea majengo ya Bunge kuvamiwa.

Hatua hiyo iliibua hisia kali mara moja huku wachanganuzi wakiitaja kuwa kinyume na sheria, wakisema kwamba jeshi linaweza kutumwa tu katika muktadha maalum na kwa idhini ya Bunge. Hata hivyo, Jumatano, Juni 26, 2024 adhuhuri, serikali iliwasilisha hoja bungeni upesi na ikapitishwa chini ya dakika 30, hivyo kuidhinisha kutumwa kwa wanajeshi kudhibiti usalama badala ya polisi wa kawaida.

Kwa kawaida, majukumu ya jeshi ni kulinda taifa dhidi ya wavamizi wanaotishia nchi. Lakini katika hatua inayoonekana kuleta mgogoro mpya, LSK Jumatano alasiri ilipata kibali cha mahakama cha kuzuia serikali kutuma jeshi kwenye barabara za miji kuzima waandamanaji.

“Agizo linatolewa kuzuia washtakiwa wawili (Afisi ya Sheria na Waziri wa Ulinzi), wafanyakazi au maajenti wao kuachilia wanajeshi kutumika katika shughuli za usalama wa nchi kulingana na Tangazo katika Gazeti Rasmi la Serikali nambari 7861 la Juni 25, 2024,” ilisema sehemu ya cheti cha agizo walichopokea LSK.

spot_img

Latest articles

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi yaanza kazi, yakaribisha wananchi kutoa maoni

Na Winfrida Mtoi Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi nchini, imesema tayari imeanza...

Urathi wa Mwalimu Nyerere usaidie kukubali kukosolewa

JUMATATU wiki hii Watanzania walikumbuka kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki...

Nimemsikiliza Gachagua, nikatamani Lowassa 2008 angelipambana vivyo

KWA zaidi ya wiki mbili sasa majirani zetu, Kenya, kumekuwa na siasa za moto....

Kukataa mgombea binafsi ni kukumbatia utumwa

HISTORIA inashuhudia kwamba wapo watumwa walikataa kuwa huru kwa sababu waliamini kwamba pamoja na...

More like this

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi yaanza kazi, yakaribisha wananchi kutoa maoni

Na Winfrida Mtoi Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi nchini, imesema tayari imeanza...

Urathi wa Mwalimu Nyerere usaidie kukubali kukosolewa

JUMATATU wiki hii Watanzania walikumbuka kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki...

Nimemsikiliza Gachagua, nikatamani Lowassa 2008 angelipambana vivyo

KWA zaidi ya wiki mbili sasa majirani zetu, Kenya, kumekuwa na siasa za moto....