Kikokotoo mafao ya Wastaafu sasa asilimia 40

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Serikali imetangaza ongezeko la malipo ya mkupuo kwa wastaafu kutoka asilimia 33 hadi asilimia 40 kwa kundi la watumishi waliokuwa wameshushwa kutoka asilimia 50 hapo awali.

Kwa muda mrefu, wafanyakazi walikuwa wakilalamikia kikokotoo cha pensheni za wastaafu kinachotumika kutokidhi hali halisi ya wanachama, wakitaka kurejeshwa kwa kanuni za zamani zilizotumika kabla ya mwaka 2017.

Msimamo huu mpya umetangazwa, Juni 13, 2024, na Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, wakati akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Amesema wastaafu waliokuwa wakipokea asilimia 25 hadi 33 sasa watapandishwa hadi asilimia 35. Pia, walioathirika na mabadiliko ya awali watakuwa sehemu ya mabadiliko haya.

“Serikali imesikia kilio cha watumishi na kufanyia kazi suala la masilahi ya wastaafu, Rais Samia ameelekeza kuongezeka kwa malipo ya mkupuo kutoka asilimia 33 hadi asilimia 40 kwa kundi la watumishi walioshushwa kutoka asilimia 50 hapo awali.

“Serikali itaendelea kuliangalia kwa karibu suala la masilahi ya wastaafu kwa kuzingatia tathmini ya uhai na uendelevu wa mifuko yetu,” amesema Dk. Mwigulu.

spot_img

Latest articles

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

Na Mwandishi Wetu, Mwanza MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung...

More like this

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...