Kanda ya Ziwa , Kaskazini vinara mauaji ya mapenzi

Kanda ya Kaskazini na Kanda ya Ziwa nchini imetajwa kuwa ni vinara wa matukio ya mauaji ya wapenzi kutokana na wivu wa mapenzi.

Taarifa ya haki za binadamu ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ya mwaka 2023 iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam jana, ilisema kuwa vifo 50 vya wapenzi kuuana vilivyoripotiwa nchini kote mwaka jana.

Katika idadi hiyo, asilimia 50 ya vifo hivyo viliripotiwa kutoka Kanda hizo. Kanda ya Kaskazini inayojumuisha mikoa ya Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga, wakati Kanda ya Ziwa inajumuisha Kagera, Mwanza, Simiyu, Shinyanga, Geita na Mara. Idadi ya vifo vingine vimeripotiwa kutoka kanda nyingine tano zilizoko nchini.

Ripoti ya haki za binadamu ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ya mwaka 2023 iliyozinduliwa jana, imeeleza kuwa mauaji hayo yameongezeka kutoka vifo 33 yaliyoripotiwa mwaka 2022.

Katika mchanganuo wa mauaji hayo, wanawake waliouawa ni 45 sawa na asilimia 90 ya vifo hivyo, wakati wanaume waliouawa ni watano sawa na asilimia 10 ya matukio hayo yanayozidi kuongezeka nchini kila mwaka, mwaka jana ukiwa umeshuhudia ongezeka vifo 17.

Taarifa hiyo inaonyesha kuwa tangu mwaka 2019 hadi mwaka jana, watu waliouawa kutokana na migogoro ya kimapenzi ni 162, licha ya idadi hiyo kuwa kubwa, inahofiwa kwamba yapo matukio mengine mengi ya mauaji ya aina hiyo ambayo yalitokea, lakini hayakutolewa taarifa.

Kwa mujibu wa LHRC asilimia 46 ya vifo vyote vilisababishwa na wivu wa mapenzi. Sababu nyingine za mauaji hayo, ni wapenzi kutokutaka kuendelea kuwa pamoja, hasa wanawake, migogoro ya ndoa na ugomvi wa mali.

Katika ripoti hiyo inayopitia matukio mbalimbali kuhusu haki za binadamu nchini kwa mwaka 2023, pia inataja mauaji ya vyombo vya dola kuua raia kuwa yalipungua kutoka vifo 10 mwaka 2022 hadi vifo 7; huku vifo vilivyosababishwa na mauaji ya imani za kishirikina vikiwa ni 164 kwa mwaka 2023; wananchi kujichukulia sheria mkononi ilisababisha vifo 461 vikipungua kutoka vifo 473 vya mwaka 2021.

Ripoti hiyo pia imezungumzia athari kwa haki za binadamu katika masuala ya ukatili wa wanawake na watoto; haki jina; ukatili dhidi ya wazee; ukatili kutokana na imani za kishirikina manusura wengi wakiwa ni wanawake; mabadiliko ya tabia nchi; utesaji; rushwa na utawala mbaya, matumizi mabaya madaraka na rasilimali za umma; haki ya mali na masuala ya bima ya afya.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...