Kanda ya Ziwa , Kaskazini vinara mauaji ya mapenzi

Kanda ya Kaskazini na Kanda ya Ziwa nchini imetajwa kuwa ni vinara wa matukio ya mauaji ya wapenzi kutokana na wivu wa mapenzi.

Taarifa ya haki za binadamu ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ya mwaka 2023 iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam jana, ilisema kuwa vifo 50 vya wapenzi kuuana vilivyoripotiwa nchini kote mwaka jana.

Katika idadi hiyo, asilimia 50 ya vifo hivyo viliripotiwa kutoka Kanda hizo. Kanda ya Kaskazini inayojumuisha mikoa ya Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga, wakati Kanda ya Ziwa inajumuisha Kagera, Mwanza, Simiyu, Shinyanga, Geita na Mara. Idadi ya vifo vingine vimeripotiwa kutoka kanda nyingine tano zilizoko nchini.

Ripoti ya haki za binadamu ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ya mwaka 2023 iliyozinduliwa jana, imeeleza kuwa mauaji hayo yameongezeka kutoka vifo 33 yaliyoripotiwa mwaka 2022.

Katika mchanganuo wa mauaji hayo, wanawake waliouawa ni 45 sawa na asilimia 90 ya vifo hivyo, wakati wanaume waliouawa ni watano sawa na asilimia 10 ya matukio hayo yanayozidi kuongezeka nchini kila mwaka, mwaka jana ukiwa umeshuhudia ongezeka vifo 17.

Taarifa hiyo inaonyesha kuwa tangu mwaka 2019 hadi mwaka jana, watu waliouawa kutokana na migogoro ya kimapenzi ni 162, licha ya idadi hiyo kuwa kubwa, inahofiwa kwamba yapo matukio mengine mengi ya mauaji ya aina hiyo ambayo yalitokea, lakini hayakutolewa taarifa.

Kwa mujibu wa LHRC asilimia 46 ya vifo vyote vilisababishwa na wivu wa mapenzi. Sababu nyingine za mauaji hayo, ni wapenzi kutokutaka kuendelea kuwa pamoja, hasa wanawake, migogoro ya ndoa na ugomvi wa mali.

Katika ripoti hiyo inayopitia matukio mbalimbali kuhusu haki za binadamu nchini kwa mwaka 2023, pia inataja mauaji ya vyombo vya dola kuua raia kuwa yalipungua kutoka vifo 10 mwaka 2022 hadi vifo 7; huku vifo vilivyosababishwa na mauaji ya imani za kishirikina vikiwa ni 164 kwa mwaka 2023; wananchi kujichukulia sheria mkononi ilisababisha vifo 461 vikipungua kutoka vifo 473 vya mwaka 2021.

Ripoti hiyo pia imezungumzia athari kwa haki za binadamu katika masuala ya ukatili wa wanawake na watoto; haki jina; ukatili dhidi ya wazee; ukatili kutokana na imani za kishirikina manusura wengi wakiwa ni wanawake; mabadiliko ya tabia nchi; utesaji; rushwa na utawala mbaya, matumizi mabaya madaraka na rasilimali za umma; haki ya mali na masuala ya bima ya afya.

spot_img

Latest articles

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

DAWASA yawaunganishiwa maji kwa mkopo wakazi wa Kibosha

Na Mwandishi Wetu Wakazi zaidi ya 100 wa Kitongoji cha Kibosha Mji Mpya wamejitokeza kuomba...

Tume uchunguzi wa matukio Oktoba 29 kukabidhi ripoti, watu 63,603 watoa maoni

Na Mwandishi Wetu TUME ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na...

More like this

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

DAWASA yawaunganishiwa maji kwa mkopo wakazi wa Kibosha

Na Mwandishi Wetu Wakazi zaidi ya 100 wa Kitongoji cha Kibosha Mji Mpya wamejitokeza kuomba...