Simba yaibadilishia kikosi Singida

Na Winfrida Mtoi

Kuelekea mechi yao na Singida Fountain Gate, Kocha Msaidizi wa Simba, Seleman Matola amesema kutokana na kucheza mechi kila baada ya siku mbili watakuwa na mabadiliko katika kikosi chao kwani baadhi ya wachezaji wamepewa mapumziko.

Matola amesema hayo leo Machi 11,2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

“Kwa sababu ukingali ‘game’ zipo kila baada ya siku mbili kwa hiyo nafikiri  kunaweza kuwa na mabadiliko kutokana na kuwapa baadhi ya wachezaji mapumziko, sisi kama benchi la ufundi tutaangalia ni nani anaweza kutufaa katika mchezo wa kesho,” amesema Matola.

Aidha amesema morali yao ipo juu na bado wana nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika ligi kuu na kuahidi kuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo.

Amekiri kuwa walifanya makosa katika michezo miwili iliyopita dhidi ya Tanzania Prisons Coastal Union  kwa kuruhusu mabao lakini wameshajirekebisha mazoezini.

Katika mchezo uliopita Wekundu wa Msimbazi hao waliifunga Coastal Union 2-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga.

spot_img

Latest articles

Balozi Nchimbi awafariji Mzee Makamba na Familia ya Mwambi

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amemtembelea...

Mtanzania achaguliwa Mkurugenzi Mtendaji Benki ya Dunia

Na Mwandishi Maalum, Washington D.C Benki ya Dunia imemchagua Mtanzania, Dk. Zarau  Kibwe, kuwa Mkurugenzi...

Shamba darasa kutoka Kenya: Hata Rais anatokwa jasho

KUNA kitu kinaitwa ‘shamba darasa’. Hili ni shamba ambalo huandaliwa na kuendeshwa kwa nia...

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi yaanza kazi, yakaribisha wananchi kutoa maoni

Na Winfrida Mtoi Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi nchini, imesema tayari imeanza...

More like this

Balozi Nchimbi awafariji Mzee Makamba na Familia ya Mwambi

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amemtembelea...

Mtanzania achaguliwa Mkurugenzi Mtendaji Benki ya Dunia

Na Mwandishi Maalum, Washington D.C Benki ya Dunia imemchagua Mtanzania, Dk. Zarau  Kibwe, kuwa Mkurugenzi...

Shamba darasa kutoka Kenya: Hata Rais anatokwa jasho

KUNA kitu kinaitwa ‘shamba darasa’. Hili ni shamba ambalo huandaliwa na kuendeshwa kwa nia...