Marubani wasinzia nusu saa ndege ikiwa angani

Mamlaka za nchini Indonesia zinachunguza tukio la marubani wawili wa ndege ya kampuni ya Batik Air ya nchini humo, waliogundulika kuwa walisinzia kwa dakika 28 wakati wa safari ya ndege yao.

Marubani hao wanaume ambao wamesimamishwa kazi kwa muda hivi sasa, walilala usingizi Januari 25, 2024 walipokuwa wakiendesha ndege kutoka mji wa Sulawesi kwenda mji mkuu wa nchi hiyo, Jakarta.

Ndege walioyokuwa wakiiendesha aina ya Airbus A320 ilipoteza mwelekeo kwa muda mfupi, lakini ilitua salama, na abiria wote 153 pamoja na wafanyakazi wanne hawakudhurika.

Vipimo vya kiafya walivyofanyiwa kabla ya safari vinaonyesha kwamba hawakuwa na tatizo lolote na hali zao ziliwaruhusu kurusha ndege.Mzunguko wa damu na mapigo ya moyo yalikuwa ya kawaida na hawakuwa wamekunywa kileo chochote.

Hata hivyo vipimo hivyo havikuweza kuthibitisha iwapo marubani hao walikuwa wamepumzika vya kutosha, alisema mtaalam wa anga za juu Alvin Lie.

Taarifa zinasema mmoja wa marubabi hao alikuwa amechoka kutokana na kukesha akisaidiana na mke wake kuwalea watoto wao pacha ambao ni wachanga.

Takriban nusu saa baada ya kupaa, Rubani Mkuu mwenye umri wa miaka 32 alimuomba rubani mwenzake kuchukua udhibiti wa ndege hiyo, akisema alihitaji kupumzika.

Kwa mujibu wa taarifa za wizara ya uchukuzi, rubani msaidizi mwenye umri wa miaka 28 alikubali lakini muda mfupi baadaye, naye alipitiwa na usingizi.

Kulingana na ripoti hiyo, mkewe alikuwa ametoka tu kujifungua watoto pacha wa mwezi mmoja na alikuwa akisaidia katika malezi ya watoto wao.

Waongoza ndege kwenye Uwanja wa ndege wa Jakarta walijaribu kuwasiliana na chumba cha marubani cha Batik Air A320, lakini hawakujibiwa.

Kimya hicho kilidumu kwa dakika 28 hadi rubani kiongozi alipoamka na kugundua kuwa rubani mwenzake naye alikuwa amepitiwa na usingizi.

Pia aligundua kuwa ndege hiyo ilikuwa imeacha njia kwa dakika kadhaa.

Baada ya kuamka, Rubani Mkuu aliitika wito kutoka Jakarta, hivyo kupata maelekezo ya mwongozo uliowezesha ndege hiyo kutua salama.

Mamlaka sasa “imeonya vikali” Batik Air kuhusu tukio hilo, na M Kristi Endah Murni, kiongozi wa usafirishaji wa anga za juu wa Indonesia, anasema Shirika hilo la ndege linapaswa kutilia maanani muda wa kupumzika kwa wafanyakazi wake.

Batik Air kwa upande wake linasema “sera yake inazingatia muda wa kutosha wa mapumziko kwa wafanyakazi wake na kuahidi kutekeleza mapendekezo yote ya kiusalama”.

Mnamo mwaka wa 2019, ndege hiyo hiyo ililazimika kutua dharura baada ya rubani kupoteza fahamu.”

spot_img

Latest articles

TRA yasifu matumizi mazuri ya fedha ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere

📌 Yasema mradi huo ni ushahidi wa thamani ya kodi za wananchi katika kuchochea...

VETA Kuongeza Vyuo Kutoka 80 hadi 152 Kufikia 2027

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetangaza mpango...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali aongoza zoezi la kutoa huduma za kisheria kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza S. Johari amewaongoza Mawakili wa Serikali...

Kliniki ya Sheria yazinduliwa jijini Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu...

More like this

TRA yasifu matumizi mazuri ya fedha ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere

📌 Yasema mradi huo ni ushahidi wa thamani ya kodi za wananchi katika kuchochea...

VETA Kuongeza Vyuo Kutoka 80 hadi 152 Kufikia 2027

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetangaza mpango...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali aongoza zoezi la kutoa huduma za kisheria kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza S. Johari amewaongoza Mawakili wa Serikali...