Marubani wasinzia nusu saa ndege ikiwa angani

Mamlaka za nchini Indonesia zinachunguza tukio la marubani wawili wa ndege ya kampuni ya Batik Air ya nchini humo, waliogundulika kuwa walisinzia kwa dakika 28 wakati wa safari ya ndege yao.

Marubani hao wanaume ambao wamesimamishwa kazi kwa muda hivi sasa, walilala usingizi Januari 25, 2024 walipokuwa wakiendesha ndege kutoka mji wa Sulawesi kwenda mji mkuu wa nchi hiyo, Jakarta.

Ndege walioyokuwa wakiiendesha aina ya Airbus A320 ilipoteza mwelekeo kwa muda mfupi, lakini ilitua salama, na abiria wote 153 pamoja na wafanyakazi wanne hawakudhurika.

Vipimo vya kiafya walivyofanyiwa kabla ya safari vinaonyesha kwamba hawakuwa na tatizo lolote na hali zao ziliwaruhusu kurusha ndege.Mzunguko wa damu na mapigo ya moyo yalikuwa ya kawaida na hawakuwa wamekunywa kileo chochote.

Hata hivyo vipimo hivyo havikuweza kuthibitisha iwapo marubani hao walikuwa wamepumzika vya kutosha, alisema mtaalam wa anga za juu Alvin Lie.

Taarifa zinasema mmoja wa marubabi hao alikuwa amechoka kutokana na kukesha akisaidiana na mke wake kuwalea watoto wao pacha ambao ni wachanga.

Takriban nusu saa baada ya kupaa, Rubani Mkuu mwenye umri wa miaka 32 alimuomba rubani mwenzake kuchukua udhibiti wa ndege hiyo, akisema alihitaji kupumzika.

Kwa mujibu wa taarifa za wizara ya uchukuzi, rubani msaidizi mwenye umri wa miaka 28 alikubali lakini muda mfupi baadaye, naye alipitiwa na usingizi.

Kulingana na ripoti hiyo, mkewe alikuwa ametoka tu kujifungua watoto pacha wa mwezi mmoja na alikuwa akisaidia katika malezi ya watoto wao.

Waongoza ndege kwenye Uwanja wa ndege wa Jakarta walijaribu kuwasiliana na chumba cha marubani cha Batik Air A320, lakini hawakujibiwa.

Kimya hicho kilidumu kwa dakika 28 hadi rubani kiongozi alipoamka na kugundua kuwa rubani mwenzake naye alikuwa amepitiwa na usingizi.

Pia aligundua kuwa ndege hiyo ilikuwa imeacha njia kwa dakika kadhaa.

Baada ya kuamka, Rubani Mkuu aliitika wito kutoka Jakarta, hivyo kupata maelekezo ya mwongozo uliowezesha ndege hiyo kutua salama.

Mamlaka sasa “imeonya vikali” Batik Air kuhusu tukio hilo, na M Kristi Endah Murni, kiongozi wa usafirishaji wa anga za juu wa Indonesia, anasema Shirika hilo la ndege linapaswa kutilia maanani muda wa kupumzika kwa wafanyakazi wake.

Batik Air kwa upande wake linasema “sera yake inazingatia muda wa kutosha wa mapumziko kwa wafanyakazi wake na kuahidi kutekeleza mapendekezo yote ya kiusalama”.

Mnamo mwaka wa 2019, ndege hiyo hiyo ililazimika kutua dharura baada ya rubani kupoteza fahamu.”

spot_img

Latest articles

Wizara ya Madini na CRDB wasaini makubaliano kurahisisha mikopo kwa wachimbaji wadogo

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Madini kupitia Tume ya Madini leo Februari 23, 2026...

Serikali yatoa Bilioni 8 kujenga Kituo cha Umeme Imalilo-Simiyu

📌 Kituo cha Imalilo kukamilika Mei 2026, kuimarisha ubora wa umeme Bariadi 📌 Serikali yatoa...

Tanzania yaandika historia Mpya: Mradi wa Umeme Jua Kishapu wakamilika

📌 Jumla ya Megawati 50 kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa ifikapo Machi 1, 2026 📌...

Kamati ya Bunge Nishati na Madini yaridhishwa na hali ya uzalishaji umeme

📌Yasema jumla ya megawati 4,400 za umeme zinazalishwa kupitia vyanzo mbalimbali 📌Yaipongeza TANESCO...

More like this

Wizara ya Madini na CRDB wasaini makubaliano kurahisisha mikopo kwa wachimbaji wadogo

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Madini kupitia Tume ya Madini leo Februari 23, 2026...

Serikali yatoa Bilioni 8 kujenga Kituo cha Umeme Imalilo-Simiyu

📌 Kituo cha Imalilo kukamilika Mei 2026, kuimarisha ubora wa umeme Bariadi 📌 Serikali yatoa...

Tanzania yaandika historia Mpya: Mradi wa Umeme Jua Kishapu wakamilika

📌 Jumla ya Megawati 50 kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa ifikapo Machi 1, 2026 📌...