Marubani wasinzia nusu saa ndege ikiwa angani

Mamlaka za nchini Indonesia zinachunguza tukio la marubani wawili wa ndege ya kampuni ya Batik Air ya nchini humo, waliogundulika kuwa walisinzia kwa dakika 28 wakati wa safari ya ndege yao.

Marubani hao wanaume ambao wamesimamishwa kazi kwa muda hivi sasa, walilala usingizi Januari 25, 2024 walipokuwa wakiendesha ndege kutoka mji wa Sulawesi kwenda mji mkuu wa nchi hiyo, Jakarta.

Ndege walioyokuwa wakiiendesha aina ya Airbus A320 ilipoteza mwelekeo kwa muda mfupi, lakini ilitua salama, na abiria wote 153 pamoja na wafanyakazi wanne hawakudhurika.

Vipimo vya kiafya walivyofanyiwa kabla ya safari vinaonyesha kwamba hawakuwa na tatizo lolote na hali zao ziliwaruhusu kurusha ndege.Mzunguko wa damu na mapigo ya moyo yalikuwa ya kawaida na hawakuwa wamekunywa kileo chochote.

Hata hivyo vipimo hivyo havikuweza kuthibitisha iwapo marubani hao walikuwa wamepumzika vya kutosha, alisema mtaalam wa anga za juu Alvin Lie.

Taarifa zinasema mmoja wa marubabi hao alikuwa amechoka kutokana na kukesha akisaidiana na mke wake kuwalea watoto wao pacha ambao ni wachanga.

Takriban nusu saa baada ya kupaa, Rubani Mkuu mwenye umri wa miaka 32 alimuomba rubani mwenzake kuchukua udhibiti wa ndege hiyo, akisema alihitaji kupumzika.

Kwa mujibu wa taarifa za wizara ya uchukuzi, rubani msaidizi mwenye umri wa miaka 28 alikubali lakini muda mfupi baadaye, naye alipitiwa na usingizi.

Kulingana na ripoti hiyo, mkewe alikuwa ametoka tu kujifungua watoto pacha wa mwezi mmoja na alikuwa akisaidia katika malezi ya watoto wao.

Waongoza ndege kwenye Uwanja wa ndege wa Jakarta walijaribu kuwasiliana na chumba cha marubani cha Batik Air A320, lakini hawakujibiwa.

Kimya hicho kilidumu kwa dakika 28 hadi rubani kiongozi alipoamka na kugundua kuwa rubani mwenzake naye alikuwa amepitiwa na usingizi.

Pia aligundua kuwa ndege hiyo ilikuwa imeacha njia kwa dakika kadhaa.

Baada ya kuamka, Rubani Mkuu aliitika wito kutoka Jakarta, hivyo kupata maelekezo ya mwongozo uliowezesha ndege hiyo kutua salama.

Mamlaka sasa “imeonya vikali” Batik Air kuhusu tukio hilo, na M Kristi Endah Murni, kiongozi wa usafirishaji wa anga za juu wa Indonesia, anasema Shirika hilo la ndege linapaswa kutilia maanani muda wa kupumzika kwa wafanyakazi wake.

Batik Air kwa upande wake linasema “sera yake inazingatia muda wa kutosha wa mapumziko kwa wafanyakazi wake na kuahidi kutekeleza mapendekezo yote ya kiusalama”.

Mnamo mwaka wa 2019, ndege hiyo hiyo ililazimika kutua dharura baada ya rubani kupoteza fahamu.”

spot_img

Latest articles

Taliss – IST Swimming Championships yawavuta wenye mahitaji maalumu

Na Winfrida Mtoi MASHINDANO ya mchezo wa kuogelea 'Taliss -IST Championship' yameanza leo Februari 14,...

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...

Wanahabari watakiwa kuweka usawa katika uandishi wa mabadiliko ya tabianchi

Na Tatu Mohamed MWAKILISHI wa kimataifa kutoka ActionAid International, Teresa Anderson, amesema ipo haja...

Dkt. Mwigulu aweka jiwe la Msingi Mradi wa Umeme Mkata

Ni ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme chenye uwezo wa MVA 60 📌Mradi...

More like this

Taliss – IST Swimming Championships yawavuta wenye mahitaji maalumu

Na Winfrida Mtoi MASHINDANO ya mchezo wa kuogelea 'Taliss -IST Championship' yameanza leo Februari 14,...

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...

Wanahabari watakiwa kuweka usawa katika uandishi wa mabadiliko ya tabianchi

Na Tatu Mohamed MWAKILISHI wa kimataifa kutoka ActionAid International, Teresa Anderson, amesema ipo haja...