Mashujaa wazitaka pointi tatu kwa Yanga

Na Winfrida Mtoi

Kueleke mchezo wao na Yanga, Kocha Mkuu wa Mashujaa FC, Mohammed Bares amesema wamejipanga kupata pointi tatu licha ya kwamba wanafahamu ugumu wa mechi hiyo.

Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utarajia kupigwa kesho Februari 8, 2024 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Katika mchezo uliopita timu hiyo ilifungwa na Simba bao 1-0 kwenye uwanja wao wa nyumbani Lake Tanganyika, Kigoma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 7,2024 jijini Dar es Salaam, Bares amesema wametoka kucheza mechi ngumu dhidi ya Simba wanaingia tena kwenye mechi ngumu lakini wamejipanga kuidhibiti Yanga.

“Ni mchezo mkubwa lakini kwenye mpira si mchezo mkubwa ni kujipanga tu na sisi tumejipanga kuidhibiti Yanga kwa sababu tunajua ina wachezaji wanaoweza kuamua matokeo,” amesema Bares.

Kwa upande wake mchezaji wa timu hiyo, Baraka Mtuwi amesema kwa kipindi hiki kila mchezo kwao wanacheza kama fainali na kuahidi kuwa hawatawaangusha mashabiki wao.

Mashujaa iliyoanza msimu huu kwa kasi hadi kukaa kwenye nafasi nne za juu mwanzoni mwa ligi hiyo, kwa sasa inashika nafasi ya 15 na alama tisa ikicheza michezo 13.

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...