Waliotafuna fedha za AMCOS Mbozi waanza ‘kuzitapika

SHILINGI milioni 170 ambazo ni sehemu ya mamilioni ya fedha zilizobainika kutafunwa baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika (AMCOS) vinane katika wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, zimerejeshwa.

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema leo bungeni Dodoma kuwa fedha hizo ni sehemu ya Sh. Milioni 294 ambazo serikali inaendelea kupambana ili kuzirejesha kwa wakulima.

Akijibu swali la mbunge wa Mbozi, George Mwenisongole, Bashe amesema mpaka sasa vyama vya ushirika 20 vimechunguzwa na vinane (8) vimebainika kufanya ubadhirifu na wahusika wamechukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa katika vyombo vya dola.

Mbunge Mwenisongole alitaka kufahamu lini serikali itaanza uchunguzi kwa vyama vya (AMCOS) ambavyo awali havikufanyiwa uchunguzi dhidi ya tuhuma za ubadhirifu kwa wakulima.

Bashe amesema unaofanywa kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika utazifikia AMCOS 98 za wilayani Mbozi na unatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2024.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...