Yanga kufanya sherehe  Mbeya, ikicheza na Prisons

Na Winfrida Mtoi

Klabu ya Yanga imepanga kufanya sherehe ya  kuadhimisha  miaka 89 tangu kuzaliwa kwake  Februari 11,2024, jijini Mbeya siku ambayo itakutana na Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 5, 2024 jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Ally Kamwe amesema tayari matukio mbalimbali kuelekea kilele cha maadhimisho hayo yameanza na kesho wanatarajia kuingia mkataba na hospitali kubwa nchini.

Amesema lengo la kuingia mkataba na hospitali hiyo ambayo hakuitaja jina ni kuweza kuwasaidia mashabiki wao katika suala la afya.

“Kesho Yanga inakwenda kusaini mkataba na hospitali kubwa sana duniani, ikiwa na lengo la kumnufaisha shabiki wetu kwenye masuala yanayohusu afya yao. Pia Jumatano tunazindua upya ofisi yetu pale Jangwani.

“Mkoa wa Mbeya umepata bahati ya kusheherekea ‘anniversary’ ya mabingwa wa kihistoria. Naomba mashabiki wote wa Yanga popote walipo wakaweke kambi Mbeya na tutazindua na nyimbo mbili kutoka kwa wasanii wakubwa,” amesema Kamwe.

spot_img

Latest articles

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi yaanza kazi, yakaribisha wananchi kutoa maoni

Na Winfrida Mtoi Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi nchini, imesema tayari imeanza...

Urathi wa Mwalimu Nyerere usaidie kukubali kukosolewa

JUMATATU wiki hii Watanzania walikumbuka kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki...

Nimemsikiliza Gachagua, nikatamani Lowassa 2008 angelipambana vivyo

KWA zaidi ya wiki mbili sasa majirani zetu, Kenya, kumekuwa na siasa za moto....

Kukataa mgombea binafsi ni kukumbatia utumwa

HISTORIA inashuhudia kwamba wapo watumwa walikataa kuwa huru kwa sababu waliamini kwamba pamoja na...

More like this

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi yaanza kazi, yakaribisha wananchi kutoa maoni

Na Winfrida Mtoi Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi nchini, imesema tayari imeanza...

Urathi wa Mwalimu Nyerere usaidie kukubali kukosolewa

JUMATATU wiki hii Watanzania walikumbuka kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki...

Nimemsikiliza Gachagua, nikatamani Lowassa 2008 angelipambana vivyo

KWA zaidi ya wiki mbili sasa majirani zetu, Kenya, kumekuwa na siasa za moto....