Yanga kufanya sherehe  Mbeya, ikicheza na Prisons

Na Winfrida Mtoi

Klabu ya Yanga imepanga kufanya sherehe ya  kuadhimisha  miaka 89 tangu kuzaliwa kwake  Februari 11,2024, jijini Mbeya siku ambayo itakutana na Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 5, 2024 jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Ally Kamwe amesema tayari matukio mbalimbali kuelekea kilele cha maadhimisho hayo yameanza na kesho wanatarajia kuingia mkataba na hospitali kubwa nchini.

Amesema lengo la kuingia mkataba na hospitali hiyo ambayo hakuitaja jina ni kuweza kuwasaidia mashabiki wao katika suala la afya.

“Kesho Yanga inakwenda kusaini mkataba na hospitali kubwa sana duniani, ikiwa na lengo la kumnufaisha shabiki wetu kwenye masuala yanayohusu afya yao. Pia Jumatano tunazindua upya ofisi yetu pale Jangwani.

“Mkoa wa Mbeya umepata bahati ya kusheherekea ‘anniversary’ ya mabingwa wa kihistoria. Naomba mashabiki wote wa Yanga popote walipo wakaweke kambi Mbeya na tutazindua na nyimbo mbili kutoka kwa wasanii wakubwa,” amesema Kamwe.

spot_img

Latest articles

Viongozi wa dini Kanda ya Magharibi waazimia kudumisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Tabora VIONGOZI wa dini katika mikoa ya Kanda ya Magharibi wameazimia...

Viongozi wa Dini Kanda ya Kusini wataka ulinzi amani, kujitokeza upigaji kura

Na Mwandishi Wetu, Lindi VIONGOZI wa dini mbalimbali kutoka mikoa ya Kanda ya Kusini wamewataka...

Lissu anyimwa dhamana, kesi yaahirishwa hadi Nov 3

Na Mwandishi Wetu Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Mradi wa Taza kufungua Soko jipya la biashara ya umeme Afrika

Na Mwandishi Wetu, Mbeya IMEELEZWA kuwa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya...

More like this

Viongozi wa dini Kanda ya Magharibi waazimia kudumisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Tabora VIONGOZI wa dini katika mikoa ya Kanda ya Magharibi wameazimia...

Viongozi wa Dini Kanda ya Kusini wataka ulinzi amani, kujitokeza upigaji kura

Na Mwandishi Wetu, Lindi VIONGOZI wa dini mbalimbali kutoka mikoa ya Kanda ya Kusini wamewataka...

Lissu anyimwa dhamana, kesi yaahirishwa hadi Nov 3

Na Mwandishi Wetu Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...