Isha Mashauzi aibukia Mtata Mtatuzi

Na Winfrida Mtoi

Mwanamuziki wa miondoko ya taarabu, Isha Mashauzi atakuwa miongoni mwa watakaoshudia a pambano la ngumi la bondia Hassan Mwakinyo lililopewa jina la Mtata Mtatuzi.

Mwakinyo anatarajiwa kupanda ulingoni Januari 27, 2024 kuzichapa na Mbiya Kanku raia wa DR Congo pambano la ubingwa wa WBO Afrika litakalopigwa Amani Complex Indoor Arena, Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuelekea visiwani humo, Isha amesema alikuwepo Ubungo Plaza Desemba 26, 2023 na kushudia vitasa hasa kwa wanawake hivyo kuamua kwenda tena Zanzibar kuona burudani hiyo.

Ameeleza kuwa lengo ni kupeana sapoti kwa sababu ngumi na muziki vyote vinakwenda pamoja.

“Ngumi ni muziki na muziki ni ngumi. Zamani tulikuwa tunaamini kwamba wanaopenda michezo hii ni wanaume tu na ni hatari lakini sasa hivj hata watoto wa kike wanafanya vizuri ndiyo maana nikaamua kuja kusapoti,” amesema Isha.

Amesema kwa hali ilivyo Tanzania itafika mbali kupitia mchezo wa ngumi, huku akiwataka mashabiki kununua tiketi ili kushuhudia mapambano hayo.

Kwa upande wake Mwakinyo amesema ameshakamilisha maandalizi na kutamba kuwa yeye ni bondia mkubwa hana mpinzani nchini.

spot_img

Latest articles

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

Jessica: CCM inajali uongozi wa vijana

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM TAIFA, Jessica Mshama...

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

More like this

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

Jessica: CCM inajali uongozi wa vijana

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM TAIFA, Jessica Mshama...

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...