Isha Mashauzi aibukia Mtata Mtatuzi

Na Winfrida Mtoi

Mwanamuziki wa miondoko ya taarabu, Isha Mashauzi atakuwa miongoni mwa watakaoshudia a pambano la ngumi la bondia Hassan Mwakinyo lililopewa jina la Mtata Mtatuzi.

Mwakinyo anatarajiwa kupanda ulingoni Januari 27, 2024 kuzichapa na Mbiya Kanku raia wa DR Congo pambano la ubingwa wa WBO Afrika litakalopigwa Amani Complex Indoor Arena, Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuelekea visiwani humo, Isha amesema alikuwepo Ubungo Plaza Desemba 26, 2023 na kushudia vitasa hasa kwa wanawake hivyo kuamua kwenda tena Zanzibar kuona burudani hiyo.

Ameeleza kuwa lengo ni kupeana sapoti kwa sababu ngumi na muziki vyote vinakwenda pamoja.

“Ngumi ni muziki na muziki ni ngumi. Zamani tulikuwa tunaamini kwamba wanaopenda michezo hii ni wanaume tu na ni hatari lakini sasa hivj hata watoto wa kike wanafanya vizuri ndiyo maana nikaamua kuja kusapoti,” amesema Isha.

Amesema kwa hali ilivyo Tanzania itafika mbali kupitia mchezo wa ngumi, huku akiwataka mashabiki kununua tiketi ili kushuhudia mapambano hayo.

Kwa upande wake Mwakinyo amesema ameshakamilisha maandalizi na kutamba kuwa yeye ni bondia mkubwa hana mpinzani nchini.

spot_img

Latest articles

Balozi Nchimbi awafariji Mzee Makamba na Familia ya Mwambi

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amemtembelea...

Mtanzania achaguliwa Mkurugenzi Mtendaji Benki ya Dunia

Na Mwandishi Maalum, Washington D.C Benki ya Dunia imemchagua Mtanzania, Dk. Zarau  Kibwe, kuwa Mkurugenzi...

Shamba darasa kutoka Kenya: Hata Rais anatokwa jasho

KUNA kitu kinaitwa ‘shamba darasa’. Hili ni shamba ambalo huandaliwa na kuendeshwa kwa nia...

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi yaanza kazi, yakaribisha wananchi kutoa maoni

Na Winfrida Mtoi Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi nchini, imesema tayari imeanza...

More like this

Balozi Nchimbi awafariji Mzee Makamba na Familia ya Mwambi

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amemtembelea...

Mtanzania achaguliwa Mkurugenzi Mtendaji Benki ya Dunia

Na Mwandishi Maalum, Washington D.C Benki ya Dunia imemchagua Mtanzania, Dk. Zarau  Kibwe, kuwa Mkurugenzi...

Shamba darasa kutoka Kenya: Hata Rais anatokwa jasho

KUNA kitu kinaitwa ‘shamba darasa’. Hili ni shamba ambalo huandaliwa na kuendeshwa kwa nia...