Mwakinyo atamba yuko fiti asilimia 98 kupanda ulingoni Zanzibar

Na Winfrida Mtoi

Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya pambano lake dhidi ya Mbiya Kanku litakalofanyika Januari 27, 2024, bondia wa Hassan Mwakinyo amesema amekamilisha maandalizi kwa asilimia 98 kilichobaki ni kupima uzito pekee.

Mwakinyo na Kanku raia wa DR Congo wanatarajiwa kupanda ulingoni katika pambano la ubingwa wa WBO Afrika litakalopigwa Amani Complex Indoor Arena, Zanzibar.

Mwakinyo amesema amejiandaa kila idara, hivyo mpizani hata akimjia kwa mtindo gani yupo tayari kupambana naye, kwani mikono ndiyo itaongea ulingoni.

Bondia huyo mwenye jina kubwa nchini, amewatoa hofu mashabiki wa masumbwi visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kuwa siku hiyo ataonesha burudani ya kuvutia ya ngumi.

Mapambano mengine yatakayopigwa siku hiyo, Hussein Itaba dhidi ya Juma Misumari wa Morogoro, Bakari H.Bakari na Seleman Hamad, Masoud Khatibu atazichapa na Yahaya Khamis, huku mwanadada Zulfa Iddi akivaana na Debora Mwenda.

spot_img

Latest articles

Kapinga azindua Kituo Mama cha gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) DAR

📌 Ni cha Pili kwa ukubwa barani Afrika, Cha Kwanza kwa ukubwa EAC 📌 Kujaza...

Mapato yasiyo ya kodi yafikia asilimia 67, OMH yadhamiria kufikia lengo la mwaka

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH), imeendelea kuonesha mafanikio...

Dkt. Biteko: Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kufikia asilimia 75 mwaka 2030

Na Mwandishi Wetu 📌 Dkt. Biteko akutana na Balozi wa Japan nchini 📌 Tanzania na...

Twange aanza kazi rasmi Tanesco

📌Aomba ushirikiano ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kunufaika na umeme wa uhakika. 📌Aahidi Kuendeleza Mazuri yaliyofanyika...

More like this

Kapinga azindua Kituo Mama cha gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) DAR

📌 Ni cha Pili kwa ukubwa barani Afrika, Cha Kwanza kwa ukubwa EAC 📌 Kujaza...

Mapato yasiyo ya kodi yafikia asilimia 67, OMH yadhamiria kufikia lengo la mwaka

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH), imeendelea kuonesha mafanikio...

Dkt. Biteko: Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kufikia asilimia 75 mwaka 2030

Na Mwandishi Wetu 📌 Dkt. Biteko akutana na Balozi wa Japan nchini 📌 Tanzania na...