Mahakama ya Kenya yaongeza muda wa amri ya kuzuia kutumwa kwa polisi nchini Haiti

Nairobi, Kenyad

Mahakama Kuu ya Kenya imeongeza muda wa amri ya kuzuia kutumwa kwa polisi hadi Haiti au nchi nyingine yoyote ikisubiri kusikilizwa zaidi.

Mapema mwezi huu mahakama ilisema walalamishi hao wameibua masuala muhimu ya kitaifa na maslahi ya umma.

Kenya ilikuwa imejitolea kuongoza kikosi cha kimataifa kwenda Haiti kusaidia kukomesha ghasia za magenge. Pia iliahidi kupeleka maafisa wake 1000 kwa misheni hiyo.

Ekuru Aukot aliyekuwa mgombeaji urais na mmoja wa walalamishi alisema katiba hailengi kutumwa kwa polisi nje ya nchi.

Aliongeza kuwa atalishtaki Baraza la Mawaziri kwa kudharau mahakama baada ya wao kuidhinisha kutumwa licha ya agizo la mahakama.

Bunge litahitaji kuidhinisha idhini hiyo kabla ya kuanza kutumwa.

Hata hivyo, timu ya wanasheria wanaowakilisha bunge la kitaifa iliambia mahakama kwamba bunge hilo haliwezi kujadili suala hilo hadi maagizo yatakapoondolewa.

Haiti imekumbwa na ghasia za magenge kwa miezi kadhaa. Kumekuwa na visa 3,000 vya mauaji na visa 1,500 vya utekaji nyara kwa ajili ya fidia kulingana na Umoja wa Mataifa.

Waziri Mkuu Ariel Henry alikuwa ametoa wito wa usaidizi wa kimataifa akisema serikali imezidiwa nguvu.

spot_img

Latest articles

TAMISA kufanya kongamano Mei 16, mwaka huu

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano...

Upanuzi wa Kituo cha Kupoza umeme Mbagala mbioni kukamilika

📌Awamu ya kwanza ya upanuzi wa Kituo Megawati 45 yakamilika 📌Asema wananchi wa Mbagala...

Rais Samia aeleza mambo ya kujifunza kutoka kwa Hayati Cleopa Msuya

Na Mwandishi Wetu Rais Samia Suluhu Hassan ameongoza mazishi ya aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa...

TFF yamfungia miaka sita Katibu Mkuu DRFA

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA),Ramadhan...

More like this

TAMISA kufanya kongamano Mei 16, mwaka huu

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano...

Upanuzi wa Kituo cha Kupoza umeme Mbagala mbioni kukamilika

📌Awamu ya kwanza ya upanuzi wa Kituo Megawati 45 yakamilika 📌Asema wananchi wa Mbagala...

Rais Samia aeleza mambo ya kujifunza kutoka kwa Hayati Cleopa Msuya

Na Mwandishi Wetu Rais Samia Suluhu Hassan ameongoza mazishi ya aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa...