Mahakama ya Kenya yaongeza muda wa amri ya kuzuia kutumwa kwa polisi nchini Haiti

Nairobi, Kenyad

Mahakama Kuu ya Kenya imeongeza muda wa amri ya kuzuia kutumwa kwa polisi hadi Haiti au nchi nyingine yoyote ikisubiri kusikilizwa zaidi.

Mapema mwezi huu mahakama ilisema walalamishi hao wameibua masuala muhimu ya kitaifa na maslahi ya umma.

Kenya ilikuwa imejitolea kuongoza kikosi cha kimataifa kwenda Haiti kusaidia kukomesha ghasia za magenge. Pia iliahidi kupeleka maafisa wake 1000 kwa misheni hiyo.

Ekuru Aukot aliyekuwa mgombeaji urais na mmoja wa walalamishi alisema katiba hailengi kutumwa kwa polisi nje ya nchi.

Aliongeza kuwa atalishtaki Baraza la Mawaziri kwa kudharau mahakama baada ya wao kuidhinisha kutumwa licha ya agizo la mahakama.

Bunge litahitaji kuidhinisha idhini hiyo kabla ya kuanza kutumwa.

Hata hivyo, timu ya wanasheria wanaowakilisha bunge la kitaifa iliambia mahakama kwamba bunge hilo haliwezi kujadili suala hilo hadi maagizo yatakapoondolewa.

Haiti imekumbwa na ghasia za magenge kwa miezi kadhaa. Kumekuwa na visa 3,000 vya mauaji na visa 1,500 vya utekaji nyara kwa ajili ya fidia kulingana na Umoja wa Mataifa.

Waziri Mkuu Ariel Henry alikuwa ametoa wito wa usaidizi wa kimataifa akisema serikali imezidiwa nguvu.

spot_img

Latest articles

Baba Levo atembelea Banda la TTCL Sabasaba, apongeza Mapinduzi ya Kidijitali

Na Mwandishi Wetu MSANII na mtangazaji maarufu nchini, Clayton Chipando maarufu kama Baba Levo,...

Takwimu za Samia ni nzito, kupotezwa watu akaze zaidi

IJUMAA ya wiki iliyopita yaani Juni 27, 2025 Rais Samia Suluhu Hassan aliweka historia...

Maonesho ya Sabasaba kufunguliwa Julai 7 na Rais Mwinyi

Na Tatu Mohamed RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinzudi, Dkt. Hussein...

TTCL Yajipambanua Kama Muunganishaji Thabiti wa Mawasiliano Sabasaba 2025

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kudhihirisha uwezo wake...

More like this

Baba Levo atembelea Banda la TTCL Sabasaba, apongeza Mapinduzi ya Kidijitali

Na Mwandishi Wetu MSANII na mtangazaji maarufu nchini, Clayton Chipando maarufu kama Baba Levo,...

Takwimu za Samia ni nzito, kupotezwa watu akaze zaidi

IJUMAA ya wiki iliyopita yaani Juni 27, 2025 Rais Samia Suluhu Hassan aliweka historia...

Maonesho ya Sabasaba kufunguliwa Julai 7 na Rais Mwinyi

Na Tatu Mohamed RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinzudi, Dkt. Hussein...