Maonesho ya Sabasaba kufunguliwa Julai 7 na Rais Mwinyi

Na Tatu Mohamed

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinzudi, Dkt. Hussein Ally Mwinyi, anatarajiwa kufungua maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam 2025, Julai 7, mwaka huu.

Maonesho hayo ambayo yalianza Juni 28, mwaka huu yatafungwa Julai 13, mwaka huu na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam baada ya kutembelea Maonesho hayo, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt Selemani Jafo alisema katika maonesho hayo yanaongozwa na kaulimbiu ‘Maonesho ya Biashara ya Kimataifa fahari ya Tanzania’ kutakuwa na washiriki 3887 kutoka nchi 23 na makampuni 386 ya kimataifa.

Aliwataka Watanzania kushiriki kwa ukubwa maonesho hayo ambayo ni makubwa zaidi kutokana na ushiriki wa mataifa mbalimbali.

“Hii ni fursa ya Watanzania kujitangaza kimataifa kutokana na kuwepo na wafanyabiashara wakaubwa Afrika, pia kutakuwa na uzinduzi wa nembo yetu ambapo tunamtarajia Naibu Waziri Mkuu, Dk. Doto Biteko, kuizindua,” alisema.

Alisema kulikuwa na makampuni zaidi ya 90 ambayo yanashindanishwa, kwa sasa yamebaki matatu na atatakiwa kubaki mmoja ambaye atatangazwa siku ya uzinduzi.

Dk. Jafo aliwaomba Watanzania kushirikiana kwa pamoja katika jambo hilo kubwa ambalo litaacha alama kubwa hapa nchini.

Alisisitiza kuwa serikali imejipanga vyema katika viwanda na biashara hivyo watahakikisha maonesho hayo yanachangia katika ukuaji wa uchumi wa taifata.

Pia, aliwasisitiza Watanzania kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi mkuu wa serikali Oktoba, mwaka huu lakini kubwa kudumisha amani ya nchi.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...