Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

TRA yakana kuhusika na kufungwa kwa baa ya THE CASK

Na Mwandishi Wetu, Media Barains

Mamla ya Mapato Tanzania (TRA) imeeleza kuwa haihusiki na kufungwa kwa baa ya The Cask ya jijini Mwanza.

Taarifa iliyotolewa leo Agosti 17, na Idara ya Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano imewataka wahusika kuwasiliana na mamlaka husika kuhusu jambo hilo.

“Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuujulisha umma kuwa, haijahusika kwa namna yoyote na ufungaji wa Bar ya THE CASK iliyopo jijini Mwanza.

“Tunaomba wahusika na umma wawasiliane na Mamlaka husika juu ya jambo hilo,” imeeleza taarifa hiyo ya TRA.

Agosti 16, mwaka huu taarifa kutoka jijini Mwanza zilidai kuwa Serikali wilayani Ilemela iliifunga baa hiyo kwa tuhuma za ukwepaji kodi kwa kipindi cha miaka miwili.

“Serikali wilayani Ilemela mkoani Mwanza imeifunga baa maarufu ya The Cask Bar & Grill ya jijini Mwanza kwa tuhuma za ukwepaji kodi kwa kipindi cha miaka miwili.

“Kwa mjibu wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Kiomono Kibamba amesema, uongozi wa baa hiyo umekwapa kodi ya Serikali na kuendesha biashara zaidi ya moja eneo hilo hilo,” ilieleza taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Taifa lina umri mkubwa, mifumo yetu iakisi ukubwa huo

Ukitafakari vema safari ya umri wa taifa letu, yapo mambo kadhaa yanayojitokeza yakiashiria kwamba...

Waziri Ndejembi awasilisha bajeti ya 2026/26, kipaumbele umeme wa uhakika nchini

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amewasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya...

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

More like this

Taifa lina umri mkubwa, mifumo yetu iakisi ukubwa huo

Ukitafakari vema safari ya umri wa taifa letu, yapo mambo kadhaa yanayojitokeza yakiashiria kwamba...

Waziri Ndejembi awasilisha bajeti ya 2026/26, kipaumbele umeme wa uhakika nchini

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amewasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya...

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...