Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

TRA yakana kuhusika na kufungwa kwa baa ya THE CASK

Na Mwandishi Wetu, Media Barains

Mamla ya Mapato Tanzania (TRA) imeeleza kuwa haihusiki na kufungwa kwa baa ya The Cask ya jijini Mwanza.

Taarifa iliyotolewa leo Agosti 17, na Idara ya Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano imewataka wahusika kuwasiliana na mamlaka husika kuhusu jambo hilo.

“Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuujulisha umma kuwa, haijahusika kwa namna yoyote na ufungaji wa Bar ya THE CASK iliyopo jijini Mwanza.

“Tunaomba wahusika na umma wawasiliane na Mamlaka husika juu ya jambo hilo,” imeeleza taarifa hiyo ya TRA.

Agosti 16, mwaka huu taarifa kutoka jijini Mwanza zilidai kuwa Serikali wilayani Ilemela iliifunga baa hiyo kwa tuhuma za ukwepaji kodi kwa kipindi cha miaka miwili.

“Serikali wilayani Ilemela mkoani Mwanza imeifunga baa maarufu ya The Cask Bar & Grill ya jijini Mwanza kwa tuhuma za ukwepaji kodi kwa kipindi cha miaka miwili.

“Kwa mjibu wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Kiomono Kibamba amesema, uongozi wa baa hiyo umekwapa kodi ya Serikali na kuendesha biashara zaidi ya moja eneo hilo hilo,” ilieleza taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...