Balozi wa Tanzania UAE awasilisha Hati za Utambulisho

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Lt. Jen. (Mst) Yacoub Hassan Mohamed amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Sheikh Mohammed Bin Zayed Al Nahyan katika Ikulu ya nchi hiyo iliyopo Mjini Abu Dhabi.

Akizungumza baada ya kupokea hati hizo, Rais Al Nahyan alimuhakikishia, Balozi Mohamed ushirikiano na Serikali yake katika kutekeleza majukumu yake nchini UAE kwa manufaa ya pande zote mbili.

Kwa upande wake Balozi Mohamed alimuahidi, Rais kuwa atahakikisha Watanzania na Waemirati wananufaika na fursa za kiuchumi zilizopo katika pande zote mbili.

Tanzania na UAE zina fursa nyingi za kushirikiana kiuchumi hususan katika sekta ya nishati ambayo UAE ni miongoni mwa nchi tajiri katika uzalishaji wa mafuta. Tanzania ina eneo kubwa la kilimo hivyo ina soko kubwa la bidhaa za Kilimo na Mifugo ambapo ushirikiano huo utawezesha uzalishaji wa kisasa na kuongeza thamani ya bidhaa.

Bidhaa zenye soko kubwa kwa Tanzania nchini UAE ni mbogamboga, matunda, nyama, korosho, karafuu, chai, karanga, asali, samaki na kahawa.

Pamoja na Umoja wa Falme za Kiarabu ubalozi huo pia unawakilisha nchi za Bahrain, Pakistan na Iran.

spot_img

Latest articles

CHELSEA BINGWA WA FIFA CWC 2025

Timu ya Chelsea imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia la Klabu kwa kuchapa...

Humphrey Polepole ajiuzulu

Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ubalozi na...

Nandy ahamasika kutangaza Nembo ya Made in Tanzania Kimataifa

Na Tatu Mohamed MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Faustina Mfinanga (Nandy), amesema elimu aliyoipata...

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

More like this

CHELSEA BINGWA WA FIFA CWC 2025

Timu ya Chelsea imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia la Klabu kwa kuchapa...

Humphrey Polepole ajiuzulu

Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ubalozi na...

Nandy ahamasika kutangaza Nembo ya Made in Tanzania Kimataifa

Na Tatu Mohamed MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Faustina Mfinanga (Nandy), amesema elimu aliyoipata...