Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Madaktari wafanikiwa kukiongezea damu kijusi ndani ya tumbo la mama

Nairobi, Kenya

Madaktari katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta nchini Kenya wamefanikiwa kutia damu kwa kijusi akiwa bado kwenye mfuko wa uzazi wa mama huyo.

Utaratibu huo wa umakini zaidi, unaojulikana kama Uhamisho wa Ndani wa Kijusi ni hatua muhimu katika matibabu ya kijusi na utaalamu wa tiba ya ndani ya mwili wa mama.

Timu ya madaktari bingwa wanne walifanya utaratibu huo wa kimatibabu ambapo chembe nyekundu za damu kutoka kwa wafadhili hudungwa ndani ya kijusi.

Uhamisho wa ndani ya mfuko wa uzazi unaweza kupendekezwa wakati kijusi kina upungufu wa damu au Anemia (hali inayopunguza seli za damu).

Madaktari hao ni pamoja na Rosa Chemwey, Flavia Ogutu, Ikol Adung’o na Kunjira Murayi, Mtaalamu wa tiba ya miale.

Walisaidiwa na Benson Nyankuru na Redempata Mumo ambao ni wauguzi, na Tony Wainaina, Afisa wa Kliniki ya Afya ya Uzazi.

Kwa kutumia kipimo cha ultrasound ili kubainisha nafasi ya kijusi na na kondo la nyuma la uzazi, daktari wa upasuaji huingiza sindano kwenye fumbatio la mama na kisha kwenye mshipa wa kitovu cha kijusi.

spot_img

Latest articles

Mandonga ampa jina jipya Kaoneka, King Class na Nasibu Ramadhani moto utawaka

Na Mwandishi Wetu Kuelekea pambano la ngumi la 'Dar Boxing Derby', bondia Karim Mandonga kama...

FCC yawahamasisha wananchi kulinda Afya na Haki zao dhidi ya Bidhaa Bandia

Na Tatu Mohamed TUME ya Ushindani (FCC) imewataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika kulinda...

PSPTB yatangaza Mitihani ya 31 ya Kitaaluma, Usajili kufungwa Agosti 15, mwaka huu

Na Tatu Mohamed BODI ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetangaza kuendesha Mitihani ya...

Ewura CCC: Wananchi wadai fidia wanapocheleweshewa kuunganishiwa maji kwa siku saba za kazi

Na Tatu Mohamed BARAZA la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji...

More like this

Mandonga ampa jina jipya Kaoneka, King Class na Nasibu Ramadhani moto utawaka

Na Mwandishi Wetu Kuelekea pambano la ngumi la 'Dar Boxing Derby', bondia Karim Mandonga kama...

FCC yawahamasisha wananchi kulinda Afya na Haki zao dhidi ya Bidhaa Bandia

Na Tatu Mohamed TUME ya Ushindani (FCC) imewataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika kulinda...

PSPTB yatangaza Mitihani ya 31 ya Kitaaluma, Usajili kufungwa Agosti 15, mwaka huu

Na Tatu Mohamed BODI ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetangaza kuendesha Mitihani ya...