Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Madaktari wafanikiwa kukiongezea damu kijusi ndani ya tumbo la mama

Nairobi, Kenya

Madaktari katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta nchini Kenya wamefanikiwa kutia damu kwa kijusi akiwa bado kwenye mfuko wa uzazi wa mama huyo.

Utaratibu huo wa umakini zaidi, unaojulikana kama Uhamisho wa Ndani wa Kijusi ni hatua muhimu katika matibabu ya kijusi na utaalamu wa tiba ya ndani ya mwili wa mama.

Timu ya madaktari bingwa wanne walifanya utaratibu huo wa kimatibabu ambapo chembe nyekundu za damu kutoka kwa wafadhili hudungwa ndani ya kijusi.

Uhamisho wa ndani ya mfuko wa uzazi unaweza kupendekezwa wakati kijusi kina upungufu wa damu au Anemia (hali inayopunguza seli za damu).

Madaktari hao ni pamoja na Rosa Chemwey, Flavia Ogutu, Ikol Adung’o na Kunjira Murayi, Mtaalamu wa tiba ya miale.

Walisaidiwa na Benson Nyankuru na Redempata Mumo ambao ni wauguzi, na Tony Wainaina, Afisa wa Kliniki ya Afya ya Uzazi.

Kwa kutumia kipimo cha ultrasound ili kubainisha nafasi ya kijusi na na kondo la nyuma la uzazi, daktari wa upasuaji huingiza sindano kwenye fumbatio la mama na kisha kwenye mshipa wa kitovu cha kijusi.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...