Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Dk. Kikwete kuwaaga wapanda mlima 61 Kampeni ya GGML KiliChallenge-2023

Na Mwandishi Wetu, Media Brain

RAIS mstaafu Dk. Jakaya Kikwete kesho Ijumaa Julai 14, 2023 anatarajiwa kuwaaga jumla ya washiriki 61 watakaopanda mlima Kilimanjaro kupitia kampeni ya ‘GGML KiliChallenge -2023’ inayolenga kukusanya fedha kwa ajili ya kutunisha Mfuko wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi (ATF) na kuendeleza mapambano ya kutokomeza Virusi Vya Ukimwi (VVU).

 Kampeni hiyo iliasisiwa mwaka 2002 na Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML kwa ushirikiano na Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Tixon Nzunda ilisema baada ya Dk. Kikwete kuwaaga washiriki hao katika lango la Machame kesho Julai 14, watapokewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu katika lango la Mweka Kibosho Julai 20 mwaka huu saa 3 asubuhi.

Aidha, akifafanua kuhusu kampeni hiyo, Makamu Rais wa AngloGold Ashanti- GGML anayeshughulikia miradi endelevu Ghana na Tanzania, Simon Shayo alisema mwaka huu jumla ya washiriki 35 watapanda mlima huo kwa njia ya kawaida ilihali washiriki 26 wataupanda mlima kwa kutumia baiskeli.

Alisema katika kampeni hiyo kutakuwa na utolewaji wa huduma bure za upimaji wa VVU, ushauri nasaha na kujitolea kutoa damu.

Mbali na kuishukuru Serikali kwa kuunga mkono kampeni hiyo iliyoasisiwa mwaka 2002, Shayo alisema  wakiwa wadau wa mapambano haya ya UKIMWI na VVU, GGML imepokea msaada ambao uliiwezesha Kili Challenge kupiga hatua kubwa hadi kufikia kuwa mfuko wa kimataifa, wenye kushirikisha wapanda mlima na waendesha baiskeli kutoka mabara yote na zaidi ya nchi 20.

Fedha hizo ambazo hukusanywa kila mwaka, hulenga kuchangia juhudi za serikali ya Tanzania katika jitihada zake kufikia malengo ya sifuri tatu yaani kupunguza kabisa kwa kufikia asilimia sifuri ya maambukizi mapya, sifuri ya unyanyapaa pamoja na sifuri katika vifo vitokanavyo na UKIMWI.

spot_img

Latest articles

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...

Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama...

More like this

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...