Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Dk. Kikwete kuwaaga wapanda mlima 61 Kampeni ya GGML KiliChallenge-2023

Na Mwandishi Wetu, Media Brain

RAIS mstaafu Dk. Jakaya Kikwete kesho Ijumaa Julai 14, 2023 anatarajiwa kuwaaga jumla ya washiriki 61 watakaopanda mlima Kilimanjaro kupitia kampeni ya ‘GGML KiliChallenge -2023’ inayolenga kukusanya fedha kwa ajili ya kutunisha Mfuko wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi (ATF) na kuendeleza mapambano ya kutokomeza Virusi Vya Ukimwi (VVU).

 Kampeni hiyo iliasisiwa mwaka 2002 na Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML kwa ushirikiano na Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Tixon Nzunda ilisema baada ya Dk. Kikwete kuwaaga washiriki hao katika lango la Machame kesho Julai 14, watapokewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu katika lango la Mweka Kibosho Julai 20 mwaka huu saa 3 asubuhi.

Aidha, akifafanua kuhusu kampeni hiyo, Makamu Rais wa AngloGold Ashanti- GGML anayeshughulikia miradi endelevu Ghana na Tanzania, Simon Shayo alisema mwaka huu jumla ya washiriki 35 watapanda mlima huo kwa njia ya kawaida ilihali washiriki 26 wataupanda mlima kwa kutumia baiskeli.

Alisema katika kampeni hiyo kutakuwa na utolewaji wa huduma bure za upimaji wa VVU, ushauri nasaha na kujitolea kutoa damu.

Mbali na kuishukuru Serikali kwa kuunga mkono kampeni hiyo iliyoasisiwa mwaka 2002, Shayo alisema  wakiwa wadau wa mapambano haya ya UKIMWI na VVU, GGML imepokea msaada ambao uliiwezesha Kili Challenge kupiga hatua kubwa hadi kufikia kuwa mfuko wa kimataifa, wenye kushirikisha wapanda mlima na waendesha baiskeli kutoka mabara yote na zaidi ya nchi 20.

Fedha hizo ambazo hukusanywa kila mwaka, hulenga kuchangia juhudi za serikali ya Tanzania katika jitihada zake kufikia malengo ya sifuri tatu yaani kupunguza kabisa kwa kufikia asilimia sifuri ya maambukizi mapya, sifuri ya unyanyapaa pamoja na sifuri katika vifo vitokanavyo na UKIMWI.

spot_img

Latest articles

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...

Mradi wa upanuzi Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kinyerezi I Extension umekamilika

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema kuwa mradi wa upanuzi...

More like this

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...