Watalii waongezeka Kilwa

Na Mwandishi wetu, Kilwa

Idadi ya watalii kutoka Mataifa mbalimbali duniani imezidi kuongezeka katika Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara kutokana na utalii wa kihistoria na kiutamaduni.

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA ),taasisi yenye dhamana ya usimamizi wa hifadhi hiyo, Februari 15,2024 ilipokea kundi la tani la watalii 119 kutoka ikiwa ni mfululizo wa safari za watalii wa nje kutembelea hifadhi hiyo kwa shughuli za utalii.

Watalii waliowasili ni kutoka katika nchi za Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Ubelgiji, Hispania na Canada wakisafirishwa na meli iitwayo Le Bougainville.

Kwa mujibu wa TAWA, hayo ni matokeo ya hatua za makusudi zilizofanywa na Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Dk.Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha sekta ya utalii nchini inakua kwa kasi baada ya kucheza filamu maarufu iitwayo Tanzania The Royal Tour.

Pia jitihada za dhati zilizofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia mamlaka hiyo kwa kuboresha miundombinu wezeshi ya utalii katika hifadhi hiyo.

spot_img

Latest articles

Waziri Katambi anatengeneza janga kubwa

MEI mwaka huu picha mjongeo ya mahojiano kati ya Inspekta Jenerali wa Polisi Mstaafu,...

DIB yawaita wananchi kupata elimu ya amana

Na Mwandishi Wetu BODI ya Bima ya Amana (DIB) imewahimiza wananchi kutembelea banda lake katika...

Waziri Mkuu: Kafulila kiongozi kijana mwenye upeo mpana

Amtaja Kama Kiongozi Kijana Mwenye Exposure ya Kimataifa Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu wa Jamhuri...

VETA Kihonda yaja na mashine ya kisasa ya kulimia

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Ufundi stadi (VETA) Kihonda, imebuni mashine...

More like this

Waziri Katambi anatengeneza janga kubwa

MEI mwaka huu picha mjongeo ya mahojiano kati ya Inspekta Jenerali wa Polisi Mstaafu,...

DIB yawaita wananchi kupata elimu ya amana

Na Mwandishi Wetu BODI ya Bima ya Amana (DIB) imewahimiza wananchi kutembelea banda lake katika...

Waziri Mkuu: Kafulila kiongozi kijana mwenye upeo mpana

Amtaja Kama Kiongozi Kijana Mwenye Exposure ya Kimataifa Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu wa Jamhuri...