Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu

Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa kushiriki Mashindano ya vilabu kwa nchi za Afrika Mashariki yatakayofanyika kuanzia kesho Juni 6 hadi 7, 2026 katika bwawa la kuogelea la Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST), Masaki jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kuhusu maandalizi ya mashindano hayo, Mkurugenzi wa Elimu na Maendeleo wa Chama cha Kuogelea Tanzania (TSA), Jeremiah Keema amesema mashindano hayo yatashirikisha jumla ya vilabu 25 kutoka nchi nne ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda na Zambia.

Keema amesema mashindano hayo yanalenga kuwapa waogeleaji chipukizi nafasi ya kuonesha vipaji vyao, kujenga uzoefu wa ushindani wa kimataifa na kuimarisha mahusiano ya michezo kati ya nchi zinazoshiriki.

Aidha, amebainisha kuwa mashindano hayo ni sehemu ya juhudi za kuendeleza mchezo wa kuogelea kwa vijana na kuandaa kizazi cha waogeleaji watakaoiwakilisha vyema Tanzania katika mashindano ya ngazi mbalimbali siku zijazo.

spot_img

Latest articles

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

Tunazidi kujisokota kwenye mtego, au tunajinasua?

TAIFA limechafukwa. Kuchafukwa huku ni kutokana na kile ambacho maseneta wawili wa Marekani, Jeanne...

Ibenge aongezewa mkataba Azam FC

Na Mwandishi Wetu Klabu ya Azam imemuongezea mkataba kocha wake, Florent Ibenge, akiendelea kusalia katika...

Mwamuzi Mtanzania kuchezesha Kombe la Dunia

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI wa Tanzania wa mpira wa miguu kwa watu wenye ulemavu, Shaban...

More like this

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

Tunazidi kujisokota kwenye mtego, au tunajinasua?

TAIFA limechafukwa. Kuchafukwa huku ni kutokana na kile ambacho maseneta wawili wa Marekani, Jeanne...

Ibenge aongezewa mkataba Azam FC

Na Mwandishi Wetu Klabu ya Azam imemuongezea mkataba kocha wake, Florent Ibenge, akiendelea kusalia katika...