Na Mwandishi Wetu
SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za kujieleza kwa wabunge walikwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys bila kibali katika fainali za AFCON -17.
Zungu amesema hayo leo Juni 4, 2026 bungeni Dodoma na kuielekeza Ofisi ya Katibu wa Bunge kuwaandikia barua za kujieleza kwa nini wamevunja kanuni za kibunge za kutoka nje ya nchi bila kuwa na kibali cha ofisi ya Spika.
Amesema wabunge hao wakishindwa kuleta majibu ndani ya siku hizo, watachukuliwa hatua za kinidhamu kulingana na kanuni.
Amebainisha kuwa kumekuwa na utoro usiovumilika bungeni, ambapo baadhi ya wabunge wanaomba vibali wakisema wanakwenda majimboni lakini wanakwenda nje ya nchi.


