Na Winfrida Mtoi
Timu ya Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa na michezo miwili ya Kalenda ya FIFA dhidi ya Uganda na Rwanda, ambapo kipa wa kikosi hicho Aishi Manula amesema haitakuwa rahisi.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 1, 2026 katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam wanapofanyika mazoezi, Manula amesema timu hizi zina upinzani mkubwa zinapokutana kutokana na ujirani.
Amebainisha kuwa michezo inayokutanisha timu za ukanda mmoja huwa hazitabiriki kwa sababu hakuna timu inayokubali unyonge mbele ya jirani yake, hali inayoongeza presha na uzito wa michezo hiyo.

”Nadhani ujirani tulionao ndio utakaosababisha mechi ziwe ngumu zaidi kwa sababu kila mmoja anahitaji kupata ushindi ili kuendelea kujiona yuko kwenye nafasi bora zaidi ya mwenzake,” amesema.
Taifa Stars itavaana na Uganda nyumbani Juni 5, kisha Rwanda Juni 9, 2026


