Mafwele apigwa marufuku kuingia Marekani

Na Mwandishi Wetu

UBALOZI wa Marekani nchini Tanzania leo 21 Mei 2026, umetangaza kuwa Serikali ya Marekani imemwekea vikwazo kwa kumzuia kuingia nchini humo,  Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi Tanzania (SACP) Faustine Mafwele kwa madai ya kuhusika katika ukiukaji mkubwa wa Haki za Binadamu.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio, Marekani imesema inazo taarifa za kuaminika zinazomuhusisha Mafwele na vitendo vya ukandamizaji pamoja na vitendo vya ukiukaji wa Haki za Binadamu.

Taarifa hiyo imesema vikwazo hivyo ni sehemu ya juhudi zake za kuwawajibisha watu wanaotuhumiwa kukandamiza haki za msingi za wananchi ambapo chini ya vikwazo hivyo Mafwele hatoruhusiwa kuingia Marekani.

Marekani imedai kuwa hatua hiyo imetokana na taarifa za uchunguzi zinazohusiana na matukio ya mwaka 2025, ambapo baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi Tanzania waliwakamata, kuwatesa na kuwafanyia ukatili wanaharakati.

Wanaharakati hao ni Agather Atuhaire wa Uganda na mwanaharakati wa Kenya, Boniface Mwangi, walipokuwa jijini Dar es Salaam kufuatilia kesi ya uhaini inayomkabili kiongozi wa upinzani, Tundu Lissu.




spot_img

Latest articles

Tanesco yaendelea kuwaelimisha wanaofanya shughuli za kiuchumi kwenye miundombinu ya umeme

📌Ni katika muendelezo wa ukaguzi wa miundombinu ya umeme Dar es salaam 📌Yatoa rai kwa...

‎DAWASA yapeleka agenda ya kudhibiti upotevu wa maji Pwani

Na Mwandishi Wetu MAPAMBANO dhidi ya upotevu wa maji yamepokelewa vyema na uongozi wa...

Msaidizi wa Lissu apatikana na pingu mkononi, aeleza kilichomkuta

Na Mwandishi Wetu NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, Amani...

Tanzania yataka ushirikiano imara na kuvuka mipaka kutokomeza maralia 

Na John Mapepele, Geneva, Uswisi  WAZIRI wa Afya wa Tanzania, Mohamed Mchengerwa, ametoa wito wa...

More like this

Tanesco yaendelea kuwaelimisha wanaofanya shughuli za kiuchumi kwenye miundombinu ya umeme

📌Ni katika muendelezo wa ukaguzi wa miundombinu ya umeme Dar es salaam 📌Yatoa rai kwa...

‎DAWASA yapeleka agenda ya kudhibiti upotevu wa maji Pwani

Na Mwandishi Wetu MAPAMBANO dhidi ya upotevu wa maji yamepokelewa vyema na uongozi wa...

Msaidizi wa Lissu apatikana na pingu mkononi, aeleza kilichomkuta

Na Mwandishi Wetu NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, Amani...