Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu

KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la wachezaji  na maofisa wa benchi la ufundi kukataa kutumia chumba rasmi cha kuvalia katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo,  badala yake kutumia nyumba iliyopo nje ya uwanja huo upande wa pili wa barabara.

Tukio hilo lilitokea Mei 3, 2026 wakati wa mchezo wa Derby  ya Kariakoo dhidi ya Simba uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2.

Kwa mujibu taarifa ya  Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Tanzania iliyotolewa leo Mei 11, 2026 na  Bodi ya Ligi  (TPLB), kitendo hicho ni ukiukwaji wa Kanuni za Ligi Kuu kuhusu taratibu za mchezo.

Mbali na adhabu hiyo, Yanga pia imepewa onyo kali baada ya kuchelewa kuwasili uwanjani kwa mchezo huo, ikifika saa 10:35 alasiri badala ya saa 10:30 alasiri kama kanuni zinavyotaka.

Katika hatua nyingine, Meneja wa Yanga, Walter Harson, amefungiwa michezo mitatu pamoja na kutozwa faini ya Sh milioni moja kwa kosa la kumsukuma mchezaji wa Simba, Clatous Chama, wakati wa mchezo huo.

spot_img

Latest articles

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...

More like this

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...