Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu

MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Miko, jijini Dar es Salaam.

Taarifa za kifo cha Kambi zimethibitishwa na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Rajabu Amir, akiaeleza kuwa marehemu alipata changamoto ya kiafya ghafla alipokuwa katika majukumu yake ya kikazi.

Marehemu Kambi aliyekuwa akijulikana pia kwa jina la Ramsey ni mmoja wa wasanii wakongwe waliacha alama katika sanaa ya maigizo nchini kutokana na kuigiza filamu nyingi na kusaidia kukuza vipaji vichanga.

Miongoni mwa filamu alizoigiza ni Binti Yangu ambayo ni yake mwenyewe, nyingine ni Simu Ya Kifo, Binti Nusa, Babu Seya, Kipusa, The Lost Twins,Kipuri, Honey Moon, Surprise, Ripple of Tears, Miss Call na Romance.

Kabla ya kuingia katika sanaa ya uigizaji,marehemu Kambi aliwahi kucheza soka akiitumikia kilabu ya Yanga.

Wakati huo huo msanii wa muda mrefu wa Bongo Flava, Selemani Mvamba maarufu Spack, naye amefariki dunia leo 27 Aprili 2026 nyumbani jijini Dar es Salaam.

spot_img

Latest articles

Watu 37 washikiliwa kwa makosa ya mtandao

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limewakamata watu 37 kwa...

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

Rais Samia aahidi kuunda chombo cha upelelezi kubaini wahusika wa matukio ya uhalifu Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema kitaundwa chombo maalumu cha upelelezi kitakachoshughulikia masuala...

Jaji Chande: Katiba mpya, ugumu wa maisha vilichochea ghasia za uchaguzi 2025

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya vurugu yaliyotokea wakati na...

More like this

Watu 37 washikiliwa kwa makosa ya mtandao

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limewakamata watu 37 kwa...

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

Rais Samia aahidi kuunda chombo cha upelelezi kubaini wahusika wa matukio ya uhalifu Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema kitaundwa chombo maalumu cha upelelezi kitakachoshughulikia masuala...