Waliotafuna fedha za AMCOS Mbozi waanza ‘kuzitapika

SHILINGI milioni 170 ambazo ni sehemu ya mamilioni ya fedha zilizobainika kutafunwa baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika (AMCOS) vinane katika wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, zimerejeshwa.

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema leo bungeni Dodoma kuwa fedha hizo ni sehemu ya Sh. Milioni 294 ambazo serikali inaendelea kupambana ili kuzirejesha kwa wakulima.

Akijibu swali la mbunge wa Mbozi, George Mwenisongole, Bashe amesema mpaka sasa vyama vya ushirika 20 vimechunguzwa na vinane (8) vimebainika kufanya ubadhirifu na wahusika wamechukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa katika vyombo vya dola.

Mbunge Mwenisongole alitaka kufahamu lini serikali itaanza uchunguzi kwa vyama vya (AMCOS) ambavyo awali havikufanyiwa uchunguzi dhidi ya tuhuma za ubadhirifu kwa wakulima.

Bashe amesema unaofanywa kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika utazifikia AMCOS 98 za wilayani Mbozi na unatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2024.

spot_img

Latest articles

NIDA yawasajili watu wenye mahitaji maalum Temeke

Na Tatu Mohamed KATIKA kuadhimisha Siku ya Utambulisho Duniani, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)...

Mkurugenzi Mkuu Dawasa Mtaa kwa Mtaa kukagua huduma za maji

Na Mwandishi Wetu AFISA Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira...

Afariki kwa kuchomwa kisu kisa Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu Mabishano ya  ushabiki wa  Yanga na Simba yamesababisha kifo cha mwanaume mmoja...

Simba, Yanga zaondoka nchini

Na Winfrida Mtoi Timu za Simba na Yanga leo zimeondoka nchini leo kwa ajili ya...

More like this

NIDA yawasajili watu wenye mahitaji maalum Temeke

Na Tatu Mohamed KATIKA kuadhimisha Siku ya Utambulisho Duniani, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)...

Mkurugenzi Mkuu Dawasa Mtaa kwa Mtaa kukagua huduma za maji

Na Mwandishi Wetu AFISA Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira...

Afariki kwa kuchomwa kisu kisa Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu Mabishano ya  ushabiki wa  Yanga na Simba yamesababisha kifo cha mwanaume mmoja...